Henri Morse

Henri Morse, S.J. (Brome, Suffolk, Uingereza, 1595 – Tyburn, London, 1 Februari 1645) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki ambaye alifukuzwa nchini na mfalme mara mbili, lakini akarudi kufanya uchungaji hadi alipofungwa gerezani na, baada ya kuadhimisha Misa, aliuawa kikatili na serikali ya Uingereza [1].
Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri tarehe 15 Desemba 1929 halafu Papa Paulo VI tarehe 25 Oktoba 1970 alimtangaza kuwa mtakatifu mfiadini pamoja na wenzake 39[2].
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Henri alikuwa Mkristo wa Kanisa la Anglikana kabla hajajiunga na Kanisa Katoliki nchini Ufaransa alipomfuata ndugu yake Wiliamu aliyekuwa seminarini.
Baada ya kurudi Uingereza, alifungwa miaka minne kwa imani yake mpya, halafu akaweza kurudi bara kwa kengo la kupata upadrisho na hatimaye kufanya uchungaji usioruhusiwa na serikali ya nchi yake.
Baada ya kupadrishwa Roma alirudi kwao (1624) na tauni ilipozuka alihudumia waathirika huko Newcastle-upon-Tyne halafu York Castle. Katikati alifungwa halafu akajiunga na Wajesuiti. Baada ya miaka mitatu gerezani aliachiwa na kufukuzwa nchini, hivyo akafanya uchungaji Uholanzi.
Mwaka 1633 alirudi Uingereza akapatwa na tauni katika kuhudumia tena waathirika, akapona. Mwaka 1636 akakamatwa tena kwa imani yake lakini aliachiwa mwaka uliofuata akahama nchi kwa muda hadi mwaka 1643. Baada ya kufanya utume wake Uingereza kwa mwaka mmoja na nusu tena aliuawa kwa kuchanwachanwa kikatili chini ya sheria.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/39320
- ↑ Malcolm Pullan (30 April 2008). The Lives and Times of Forty Martyrs of England and Wales 1535 - 1680. Athena Press. pp. xvii–xxiai. ISBN 978-1-84748-258-7.
- ↑ Martyrologium Romanum
Marejeo ya Kiswahili
[hariri | hariri chanzo]- Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 33-34
Marejeo ya lugha nyingine
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Catholic Forum
- Catholic Church of St. Henry Morse Ilihifadhiwa 20 Januari 2021 kwenye Wayback Machine.
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |