Hadja Fatimata Ouattara
Hadja Fatimata Ouattara (alizaliwa Sanon) ni mwanasiasa kutoka Burkina Faso aliyewahi kuwa Waziri wa Uchumi wa Kidijitali na Maendeleo ya Posta kuanzia Februari 2017 hadi Januari 2022.
Maisha ya awali na elimu
[hariri | hariri chanzo]Ouattara alisoma katika Sainte-Marie College katika mtaa wa Bobo-Dioulasso wa Tounouma na ana shahada ya uhandisi wa kompyuta kutoka Polytechnic University of Bobo-Dioulasso pamoja na Shahada ya Uzamili (Masters) katika mitandao ya kompyuta na vyombo vya habari vya digital kutoka Kituo cha Kimataifa cha Masomo ya Juu ya Teknohama (International Centre for Applied Advanced Studies) kilichoko Humber College nchini Canada.[1][2]
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Mwaka 2005, Ouattara aliteuliwa kuwa webmaster wa Mtandao wa Usimamizi wa Maarifa wa Burkina na kuunda Shirikisho la Burkinabè la Linux na Programu Huria. Alikuwa Mshauri wa Kiufundi katika Wizara ya TEHAMA. Pia alifanya kazi kwa mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali na ni mwanachama wa kuanzisha wa Mtandao wa Programu Huria wa Afrika. Wakati wa kipindi cha mpito baada ya Mapinduzi ya Burkina Faso 2014, alishikilia wadhifa wa Katibu Teknohiki katika Wizara ya Huduma za Umma.
Ouattara aliteuliwa kuwa Waziri wa Uchumi wa Kidijitali na Maendeleo ya Posta na Rais Roch Marc Christian Kaboré tarehe 23 Februari, 2017.[3]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Hadja Fatimata Ouattara/Sanon: une passionnée des TIC au ministère du Développement de l'Economie numérique et des Postes". Les Echos du Faso (kwa French). 21 Februari 2017. Iliwekwa mnamo 24 Novemba 2017.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link) - ↑ "Burkina Faso : Qui est Mme Adja Fatimata Ouattara, la nouvelle ministre en charge des TIC". TIC Mag (kwa French). 23 Februari 2017. Iliwekwa mnamo 24 Novemba 2017.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link) - ↑ Kindo, Noufou (23 Februari 2017). "Ministère des TIC : Qui est Hadja Fatimata Ouattara/Sanon ?" (kwa French). Burkina 24. Iliwekwa mnamo 24 Novemba 2017.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link)
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Hadja Fatimata Ouattara kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |