Gyude Bryant

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

'

Gyude Bryant
Bryant mwaka 2004
Amezaliwa17 Januari 1949
Amefariki16 Aprili 2014
Kazi yakemwanasiasa na mfanyabiashara


Charles Gyude Bryant (17 Januari 1949 - 16 Aprili 2014) alikuwa mwanasiasa na mfanyabiashara nchini Liberia.

Aliwahi kuwa mwenyekiti wa serikali ya mpito ya Liberia kuanzia tarehe 14 Oktoba mwaka 2003 hadi tarehe 16 Januari mwaka 2006. Kuwepo kwa serikali ya mpito ilikuwa sehemu ya makubaliano ya amani ya kumaliza vita ya pili ya wenyewe kwa wenyewe ya Liberia, ambayo ilipamba moto katika kipindi Waliberia wanaungana kwa ajili ya maridhiano na demokrasia kumpinga rais Charles Taylor (mwanasiasa wa Liberia) mwaka 1999.

Bryant hapo awali alikuwa mfanyabiashara na alichaguliwa kuwa mwenyekiti kwa sababu alionekana kutoegemea upande wowote kisiasa na hivyo kukubalika kwa kila kundi linalopigana ikijumuisha chama cha LURD, Movement for Democracy in Liberia (MODEL), na watiifu wa rais wa zamani Taylor. Alikuwa mshiriki mashuhuri wa kanisa la Episcopal la Liberia, na alikuwa mkosoaji wa serikali za Samuel Doe mnamo (19801990) na Taylor mnamo (1997-2003).

Ellen Johnson Sirleaf alishinda uchaguzi mkuu wa Liberia wa mwaka 2005 na kuchukua ofisi Januari mwaka 2006, akimrithi Bryant.

Alifariki mnamo tarehe 16 Aprili mwaka 2014 katika kituo cha afya cha John F. Kennedy (Liberia) huko Monrovia.[1][2]

Binafsi[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa huko Monrovia mwanzoni mwa enzi za William Tubman, mama yake Bryant alikuwa mzaliwa wa walowezi na baba yake alikuwa mwanachama wa Watu wa Grebo. Alifuzu mafunzo yake katika Chuo Kikuu cha Cutington mwaka 1972, na mwaka 1974alimuoa Rosilee Williams wa zamani;walibahatika kupata watoto wawili ambao ni Cheryl na Charles.

Bryant pia alikua na mtoto wakiume aliyejulikana kwa jina la Charles Mleh. Kabla ya kuwa mwenyekiti wa serikali ya mpito, alikuwa mfanyabiashara aliyefanikiwa, akiendesha kampuni iliyosambaza mashine kwa ajili ya bandari huru ya Monrovia, na alikuwa mwenyekiti wa chama cha Liberian Action Party.[3]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Charles Gyude Bryant, Former Liberia Interim President is Dead", 16 April 2014. Retrieved on 2022-02-22. Archived from the original on 2014-04-17. 
  2. Butty, James. "Gyude Bryant, Liberia's Sixth Transitional Leader, Dies at 65", April 17, 2014. 
  3. Weiner, Tim. "A Man Without Enemies: Charles Gyude Bryant". The New York Times 2003-08-22. Accessed 2013-01-26.