Great Dividing Range

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Milima ya Dividing Range.
Ramani ya Australia; rangi njano inaonyesha Great Dividing Range.

Great Dividing Range (kwa maana Mgawanyiko Mkubwa) au Nyanda za Juu za Mashariki, ndiyo safu ya milima kubwa zaidi kwenye bara la Australia [1]. Inaenea kwa kilomita 3,500 sambamba na pwani ya mashariki la Australia, kuanzia Queensland ikipita Victoria hadi magharibi mwa Victoria. Upana wa masafa unatofautiana kutoka karibu km 160 hadi zaidi ya km 300.

Eneo lote si safu moja ya milima tu; kuna safu mbalimbali, milima, nyanda za juu na mitelemko. Kwenye sehemu kadhaa nchi ni karibu tambarare bila miinuko mikubwa, pengine kuna milima mikali inayofikia kimo cha mita 1,600.

Kilele cha juu ni Mlima Kosciuszko wenye mita 2,228 uliopo kwenye milima ya Snowy ("milima ya theluji").

Safu za Great Dividing Range zimepata jina kwa sababu zilikuwa kizuizi cha mawasiliano kati ya mashariki ya Australia ambako idadi kubwa ya wananachi wote inapatikana, na sehemu nyingine za bara.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. The Great Dividing Range is the third longest mountain range of mountain ranges above sea level. The underwater mid-ocean ridge is the longest of the world's mountain ranges.
Makala hii kuhusu maeneo ya Australia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Great Dividing Range kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.