Nenda kwa yaliyomo

Grace Adams

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Grace Adams (alizaliwa 2 Novemba, 1995) ni mchezaji wa mpira wa miguu wa wanawake wa kulipwa kutoka nchini Ghana anayekipiga kama kiungo wa kati na beki wa kati kwa klabu ya FC Nasaf inayoshiriki Ligi ya Wanawake ya Uzbekistan, pamoja na timu ya taifa ya wanawake ya Ghana.

Alisoma na kucheza mpira wa miguu katika Chuo Kikuu cha South Florida nchini Marekani kati ya mwaka 2015 na 2019, na sasa ana shahada ya masuala mbalimbali ya kijamii. Aliwahi kuwa nahodha wa timu ya vijana ya wanawake ya Ghana, Black Princesses (chini ya umri wa miaka 20), na kuwaongoza katika Michuano ya Dunia ya Wanawake chini ya miaka 20 yaliyofanyika Kanada mwaka 2014.[1]

  1. "Police find their target to finish on top". Modern Ghana (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2021-02-07.
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Grace Adams kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.