Gladys Wanga
Mandhari
Gladys Atieno Wanga (aliyekuwa Nyasuna; alizaliwa 7 Machi 1981) ni mwanamke kisiasa kutoka Kenya ambaye kwa sasa ni Gavana wa Kaunti ya Homa Bay. Yeye ndiye mwanamke wa kwanza kutoka Mkoa wa Magharibi wa Kenya kuchaguliwa kuwa gavana, na mmoja kati ya wanamke saba walioteuliwa kuwa magavana katika Chaguzi za Jumla za Kenya 2022.[1] Awali alihudumu kama Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Homa Bay kuanzia 2013 hadi 2022. Anao mume ambaye pia alikuwa Mwenyekiti Asiyo Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nguvu na Petroli (EPRA), George Wanga.[2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Owino, Anthony (2019-06-25). "Find Out What Women Reps Do". Kenyans.co.ke. Iliwekwa mnamo 2024-04-16.
- ↑ Agencies for Kenya Online News. "Homa Bay Governor Gladys Wanga's Husband Lands Government Job". Kenya Online News. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 11 Februari 2025. Iliwekwa mnamo 22 Januari 2025.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Gladys Wanga kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |