Ghuba ya Chaka-Chake
Mandhari

Ghuba ya Chake-Chake ni sehemu kubwa iliyochongwa kiasili katika pwani ya magharibi ya kati ya Kisiwa cha Pemba, mojawapo ya visiwa viwili vikuu vya Funguvisiwa la Zanzibar linalounda Tanzania.
Jiografia
[hariri | hariri chanzo]Mji wa Chake-Chake, ambao ni moja ya vituo vikuu vya watu kisiwani humo, uko katika pwani ya kati ya ghuba hii.
Ghuba hii si pana sana, kwani inanyooka kwa takribani kilomita tano kutoka kaskazini hadi kusini, lakini ni yenye kina kirefu. Imezungukwa na rasi mbili ndefu: Rasi Tundua upande wa kusini na Rasi Mkumbuu upande wa kaskazini. Rasi ya pili ilikuwa mahali pa mojawapo ya makazi ya awali muhimu kisiwani humo, Magofu ya Qanbalu, ambayo kwa sasa ni magofu tu.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Finke, J. (2006) The Rough Guide to Zanzibar (Toleo la 2). New York: Rough Guides.
| Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Ghuba ya Chaka-Chake kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |