Gülçiçek Hatun
Gülçiçek Hatun (pia anajulikana kama Gökçiçek Hatun,[1]; 1335 - 1400) alikuwa mwanamke Mgiriki kutoka Bitinia ambaye alikuja kuwa suria wa Sultani wa Milki ya Osmani Murad I, na baadaye akawa Valide Hatun (mama wa sultani) wa mwanawe Bayezid I.[2]
Wasifu
[hariri | hariri chanzo]Kwa mujibu wa simulizi za jadi, Gülçiçek alikuwa suria wa Aslan Bey, mmoja wa wakuu wa Ufalme wa Kiislamu wa Anatolia wa Karasids. Alitekwa wakati Orhan alipoutawala ufalme huo (mwaka 1344) na kisha akaingizwa katika haremi ya sultani. Mnamo mwaka 1359, akawa suria wa mwana wa Orhan, Murad, alipofikia umri wa utu uzima.[3]
Alimzalia Murad wana wawili: Bayezid I na Yahşi Bey. Alimteua mwanawe Yahşi kuwa mdhamini wa hati ya wakfu aliyoiweka kwa ajili ya monasteri ya dervishi. Katika kipindi cha uhai wake, alianzisha taasisi ya kidini na kijamii iliyoonyesha wazi ucha-Mungu wake wa Kiislamu. Kwa mapato ya wakfu huo, alijenga msikiti akiwa ndiye suria wa kwanza wa Othmania kujenga msikiti na pia kaburi huko Bursa, ambako alizikwa alipofariki dunia mwaka 1400.[4][5]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Goodwin, Godfrey (2014). The Private World of Ottoman Women, p. 120
- ↑ "Sultan Yıldırım Beyezid Han". Republic of Turkey Ministry of Culture and Tourism. Archived from the original on August 13, 2014. Retrieved 2009-02-06.
- ↑ Leslie P. Peirce (1993). "Wives and Concubines: The Fourteenth and Fifteenth Centuries". The Imperial Harem: Women and Sovereignty in the Ottoman Empire. Oxford University Press. p. 36. ISBN 978-0-195-08677-5.
- ↑ The Nature of the Early Ottoman State, Heath W. Lowry, State University of New York Press (SUNY Press), p. 153
- ↑ History of the Ottoman Empire and Modern Turkey, Stanford Jay Shaw, Cambridge University Press, p. 28