Fred Guttenberg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Fred Guttenberg (alizaliwa 24 Disemba, 1965) ni mwanaharakati wa Kimarekani dhidi ya unyanyasaji wa bunduki. Binti yake mwenye umri wa miaka 14 Jaime Guttenberg[1] aliuawa katika ufyatuaji risasi katika Shule ya awali ya Stoneman Douglas mnamo 14 Februari, 2018. Kijana wake, Jesse, ambaye pia ni mwanafunzi wa shule hiyo, alikimbia kutoka katika mashambulizi na kukutana naye katika duka la karibu[2]. Alijifunza kuhusu kifo cha binti yake kutoka kwa rafiki ambaye ni afisa wa SWAT[3]. Jessica McBride, wa tovuti ya Heavy, alimweleza kama "mojawapo ya sauti kali zaidi za mabadiliko ya sheria za bunduki kuhusu ufyatuaji risasi."[4]

Uanaharakati[hariri | hariri chanzo]

Siku baada ya mashambulizi ya risasi, Guttenbeg alizungumza kuhusu udhibiti wa bunduki, akisema "Usiniambie hakuna kitu kama ukiukwaji wa matumizi ya bunduki. Ilitokea Parkland"[5]. Mbele ya ukumbi wa jiji wa CNN unaoonyeshwa kitaifa alimkosoa Rais kwa kutosema kua bunduki ni tatizo katika vikao cha kusikiliza vya Ikulu ya Marekani, akisema "Binti yangu aliwindwa wiki iliyopita" na "Nimekasirika"[6][7]. Wakati wa onyesho la ukumbi wa mji wa CNN alikabiliana na Seneta wa Florida Marco Rubio kwa msimamo wake kuhusu bunduki.[8][9]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Jessica McBride (2018-02-21). "Fred Guttenberg, Jaime’s Father: 5 Fast Facts You Need to Know". Heavy.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2022-08-02. 
  2. https://www.marieclaire.com/politics/amp18922594/parkland-shooting-victim-father-fred-jaime-guttenberg-true-story/
  3. "Fred Guttenberg will not sit down: Florida father demands gun reform". the Guardian (kwa Kiingereza). 2018-03-11. Iliwekwa mnamo 2022-08-02. 
  4. Jessica McBride (2018-02-21). "Fred Guttenberg, Jaime’s Father: 5 Fast Facts You Need to Know". Heavy.com (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2022-08-02. 
  5. "Who Is Fred Guttenberg? Marco Rubio Was Addressed Head-On By A Parkland Victim's Dad". Bustle (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-08-02. 
  6. Father of victim: My daughter was hunted - CNN Video, iliwekwa mnamo 2022-08-02 
  7. David Choi. "'I am enraged': Father of Parkland shooting victim blasts the listening session Trump held with mass-shooting survivors". Business Insider (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2022-08-02. 
  8. Victim's father, Sen. Rubio in heated exchange - CNN Video, iliwekwa mnamo 2022-08-02 
  9. Josiah Ryan (2018-02-22). "Father of teen slain in Florida school massacre slams Rubio on gun stances | CNN Politics". CNN (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-08-02.