Franz Albert Seyn
Franz Albert Seyn (Aleksandrovich Zeyn}}; 27 Julai 1862 – msimu wa joto 1918) alikuwa jenerali wa Urusi aliyehudumu kama Gavana Mkuu wa Finland kuanzia tarehe 24 Novemba 1909 hadi 16 Machi 1917. Alikuwa mmoja wa watekelezaji wakuu wa Sera za Kirusi nchini Finland (Russification of Finland) kuanzia mwaka 1909 hadi 1917.
Wasifu
[hariri | hariri chanzo]Maisha ya mapema na kazi
[hariri | hariri chanzo]Seyn alitokea katika familia ya makabaila wadogo wa Gavana ya Vitebsk, ambapo baba yake, Aleksandr Seyn, alihudumu kwanza kama afisa wa jeshi na baadaye kama mtumishi wa umma. Eneo hilo lilikuwa na wakazi wa makabila ya Wabelarusi, Walithuania, Wapolandi, na Wayahudi wa madhehebu mbalimbali ya kidini. Tangu akiwa mdogo, Seyn alikuwa anafahamu jinsi serikali ya Urusi ilivyokuwa ikishughulika na makundi ya watu wachache wenye asili tofauti za kitaifa, jambo ambalo alikutana nalo tena baadaye alipohudumu kama luteni usu huko Kaukazi (Caucasus), baada ya kuhitimu shule ya maafisa na mizinga. Alidahiliwa katika Chuo cha Kijeshi cha Kifalme cha Urusi mnamo mwaka 1885, ambapo alijipambanua kwa bidii na umakini wake katika kazi.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Pertti Luntinen: F. A. Seyn 1862 - 1918 - A Political Biography of a tsarist Imperialist as Administrator of Finland, Helsinky, 1985, ISBN 951-9254-72-2, in English.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Franz Albert Seyn kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |