Fransisko Saveri Maria Bianchi
Fransisko Saveri Maria Bianchi (kwa Kiitalia: Francesco Saverio Maria Bianchi; Arpino, Lazio, 2 Desemba 1743 - Napoli, Campania, 31 Januari 1815) alikuwa padri na mtawa wa shirika la Makleri wa Mt. Paulo, maarufu kama Wabarnaba nchini Italia.
Alitangazwa na Papa Leo XIII kuwa mwenye heri tarehe 22 Februari 1893, tena mtakatifu na Papa Pius XII tarehe 21 Oktoba 1951.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].
Maisha[hariri | hariri chanzo]
Alijulikana kwa elimu yake, lakini hasa kwa juhudi zake kwa wanafunzi aliokuwanao na kwa maskini wa mji wa Napoli, hata akaitwa "Mtume wa Napoli"[2][3]. Mwenye karama za pekee, alivutia wengi kufuata kama yeye neema ya Mungu.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ Butler, Alban, Herbert Thurston, and Donald Attwater. Butler's Lives of Saints: Vol. 1.
- ↑ San Francesco Saverio Maria Bianchi (it). Santi e beati.
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |