Frank Vickerman
Mandhari
Makala hii inahitaji vyanzo zaidi ili kuwezesha kuonyesha uthibitisho. |
Frank Vickerman alikuwa mwanamme aliyeishi mwanzoni mwa karne ya 19 katika eneo la magharibi ya Yorkshire. Alimiliki kiwanda cha kuchakata pamba kilichokuwa Taylor Hill, ambacho kilishambuliwa na kundi la Luddites tarehe 15 Machi 1812. Kiwanda hicho kiliharibiwa kabisa, na pia walijaribu kukichoma moto. Frank Vickerman alilengwa na kundi hili lililopinga maendeleo ya kiteknolojia kwa sababu mashine katika kiwanda chake zilikuwa zinachukua ajira za watu, na pia kwa sababu aliwahi kushiriki katika kamati iliyokuwa inapinga harakati za Uludditi.