Frank Mill

Frank Mill (23 Julai 1958 – 5 Agosti 2025) alikuwa mchezaji wa soka wa kulipwa kutoka Ujerumani. Alikuwa miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha Timu ya Taifa ya Ujerumani Magharibi kilichoshinda Kombe la Dunia la FIFA mwaka 1990. Pia, alishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya Majira ya joto ya mwaka 1984 na 1988, ambapo alishinda medali ya shaba akiwa na timu ya Ujerumani Magharibi.[1][2]
Kazi katika Klabu
[hariri | hariri chanzo]Frank Mill, mtoto wa mfanyabiashara wa vyuma chakavu, alianza kucheza soka akiwa na umri wa miaka sita katika klabu ya mtaani ya Eintracht Essen kabla ya kujiunga na timu ya vijana ya klabu kubwa zaidi mjini Essen, Rot-Weiss Essen, mwaka 1972.
Akiwa ameanza mafunzo ya kazi ya ufundi wa maua (mamake alikuwa na duka la maua), Mill alisaini mkataba wake wa kwanza wa kulipwa na Rot-Weiss Essen mwaka 1976. Katika msimu wake wa kwanza, timu hiyo ilikuwa inacheza Bundesliga, lakini licha ya kufunga mabao matatu katika mechi 19, hakuweza kuiokoa timu kushuka daraja hadi 2. Bundesliga North.
Katika ligi hiyo ya pili, Mill alikua mshambuliaji wa kuaminika, alifunga jumla ya mabao 71 kwenye timu ya Rot-Weiss kwa misimu minne iliyofuata, yakiwemo mabao 40 katika mechi 38 tu msimu wa 1979–80. Wakati mwingine alicheza sambamba na mshambuliaji maarufu Horst Hrubesch.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Ulrich, Ron (23 Desemba 2021). "Frank Mill: The Germany striker whose name means failure - and how he found success". BBC Sport. Iliwekwa mnamo 24 Desemba 2021.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Matthias Arnhold (5 Februari 2015). "Frank Mill - Matches and Goals in Bundesliga". Rec.Sport.Soccer Statistics Foundation. Iliwekwa mnamo 13 Februari 2015.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Frank Mill kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |