Floriani wa Lorch

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro wa ukutani wa Leonhard von Brixen (1459), Taisten.

Floriani wa Lorch (alifia dini tarehe 4 Mei 304) alikuwa askari Mkristo wa Dola la Roma aliyeishi Mantem, karibu na Kirchdorf an der Krems, leo nchini Austria.

Aliposikia kwamba gavana Akwilino, wakati wa dhuluma ya kaisari Dioklesyano, amekamata Wakristo 40 mjini Lorch, alitamani kuwa nao akaenda huko. Karibu na kufika alikutana na askari wenzake akajitambulisha kuwa Mkristo, hivyo akakamatwa na kupelekwa kwa Akwilino. Huyo alijaribu kumfanya atoe sadaka kwa miungu, lakini Floriani alipokataa aliagiza apigwe mijeledi na kutupwa katika mto Enns akiwa na jiwe kubwa limefungwa shingoni[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/Detailed/51775.html
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.