Floriani wa Lorch
Mandhari

Floriani wa Lorch (alifia dini tarehe 4 Mei 304) alikuwa askari Mkristo wa Dola la Roma aliyeishi Mantem, karibu na Kirchdorf an der Krems, leo nchini Austria.
Aliposikia kwamba gavana Akwilino, wakati wa dhuluma ya kaisari Dioklesyano, amekamata Wakristo 40 mjini Lorch, alitamani kuwa nao akaenda huko. Karibu na kufika alikutana na askari wenzake akajitambulisha kuwa Mkristo, hivyo akakamatwa na kupelekwa kwa Akwilino. Huyo alijaribu kumfanya atoe sadaka kwa miungu, lakini Floriani alipokataa aliagiza apigwe mijeledi na kutupwa katika mto Enns akiwa na jiwe kubwa limefungwa shingoni[1].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.santiebeati.it/Detailed/51775.html
- ↑ Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |