Félix Díaz (cacique)
Mandhari
Félix Díaz (alizaliwa 28 Desemba 1959) ni mwanaharakati kutoka Argentina anayepigania haki za kiraia za watu wa Qom nchini humo. Yeye ni qarashé (kiongozi wa jadi) wa Potae Napocna Navogoh, inayojulikana pia kama Colonia La Primavera katika jimbo la Formosa.
Gazeti la Kihispania El País lilimtaja miongoni mwa watu 100 mashuhuri zaidi wa Ibero-Amerika mwaka 2011. Tangu Julai 2016, amekuwa rais wa Baraza la Ushauri na Ushirikishwaji la Watu wa Asili.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Félix Díaz: 'Macri no nos pidió votos, ni apoyar su candidatura'" Archived 2017-12-06 at the Wayback Machine, Diario La Nación, 3 November 2015.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Félix Díaz (cacique) kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |