Ernst Moritz Arndt
Mandhari
Ernst Moritz Arndt (26 Desemba 1769 – 29 Januari 1860) alikuwa Mjerumani mwanahistoria wa utaifa, mwandishi na mshairi. Mwanzoni mwa maisha yake alipigania kukomeshwa kwa utumwa wa kulazimishwa kwa wakulima (serfdom), na baadaye alipinga utawala wa Napoleon juu ya Ujerumani. Kutokana na misimamo yake ya kupinga Wafaransa, Arndt alilazimika kukimbilia Uswidi kwa muda.
Anahesabiwa kuwa mmoja wa waanzilishi wakuu wa utaifa wa Kijerumani wakati wa vita vya Napoleon[1] na harakati za karne ya 19 za muungano wa Ujerumani. Baada ya Carlsbad Decrees, mamlaka za kurejesha utawala wa kifalme zilimchukulia kama mchochezi wa kisiasa.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Popper, Karl (2005). Unended Quest: An Intellectual Autobiography (kwa Kiingereza). London: Routledge. uk. 7. ISBN 0-415-28589-5.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ernst Moritz Arndt kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |