Emmanuel Tutuba
Mandhari
Emmanuel Mpawe Tutuba (amezaliwa 30 Machi 1973) ni Gavana wa nane wa Benki Kuu ya Tanzania. [1]
Maisha ya Awali na Kazi
[hariri | hariri chanzo]Alimaliza masomo yake ya kidato cha sita mwaka 1994 katika Shule ya Sekondari ya Milambo iliyopo Mkoa wa Tabora, ambako alisomea somo la uchumi, jiografia na hisabati. Kuanzia mwaka 1996 hadi 1999, alisomea Stashahada ya Juu katika Mipango ya Uchumi katika Taasisi ya Tafiti za Maendeleo ya Chuo Kikuu cha Mzumbe. Baadaye, alisomea shahada ya uzamili ya MBA katika Usimamizi wa Biashara za Kampuni na kuhitimu katika chuo hicho mwaka 2001. [2]Mnamo Februari 2020, Rais John Magufuli alimteua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) wa Mkoa wa Mwanza.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Tanzanian president appoints Emmanuel Tutuba as central bank governor". Reuters. 8 Januari 2023. Iliwekwa mnamo 8 Januari 2023.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Auditor General Report on African Institute for Capacity Development" (PDF). Parliament of Kenya. 30 Juni 2019. uk. vii. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 22 Oktoba 2022. Iliwekwa mnamo 8 Januari 2023.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Emmanuel Tutuba kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |