Edwin Edeh
Edwin Isotu Edeh ni msomi, mwandishi, na mtaalamu wa afya ya umma na mazingira kutoka Nigeria. Kwa sasa anahudumu kama mshauri wa kitaifa wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa mpango wa Afya ya umma na Mazingira (PHE) nchini Nigeria.[1][2] Yeye ndiye mwandishi wa kitabu, Environmental Health: Understanding Current Issues and Solutions of the 21st Century ambacho kimekubaliwa kutumika kama kitabu cha rejea katika vyuo vikuu kadhaa barani Africa ikiwemo Chuo Kikuu cha Cavendish, Kampala na Chuo Kikuu cha Mount Kenya. [3][4] Yeye pia ameshinda tuzo mara mbili mfululizo za Mshauri Bora wa Afya Endelevu wa Nigeria (Nigeria Sustainability Health Consultant of the Year) kwa mwaka 2021 na 2022.[5]
Elimu na Kazi
[hariri | hariri chanzo]Edwin Edeh alianza masomo ya elimu yake ya juu katika Chuo cha Rivers State College of Health Science huko Port Harcourt, ambako alisoma teknolojia ya afya ya mazingira. Alipata shahada ya uzamili katika usimamizi wa mazingira kutoka Chuo Kikuu cha Port Harcourt na shahada ya uzamivu (PhD) katika usimamizi na udhibiti wa mazingira kutoka Chuo Kikuu cha Nigeria. Edeh ana cheti cha Global Health and Humanitarian kutoka Chuo Kikuu cha Manchester na cheti cha Interprofessional Health Informatics kutoka Chuo Kikuu cha Minnesota. Yeye ni mwanachama kitaaluma wa Nigeria Environment Society (NES), Mwanachama wa Taasisi ya Kiafrika ya Wataalamu wa Afya ya Umma (AIPHP), Mtaalamu wa Afya ya Mazingira aliye na leseni ya EHORECON na mshauri aliyeidhinishwa wa usimamizi wa Taasisi za Ushauri za Baraza la Kimataifa la Usimamizi, Zurich.[6]
Edeh alianza kazi yake kama afisa wa afya ya mazingira ya umma huko Oyorokoto, Andoni, Jimbo la Rivers, mojawapo ya makazi makubwa ya wavuvi katika Afrika Magharibi. Alifundisha katika Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Rivers State, Port Harcourt kabla ya kujiunga na WHO kama mtaalam wa kiufundi wa afya ya umma na mazingira na mshauri wa kitaifa wa Nigeria. Mnamo mwaka wa 2018, aliratibu utekelezaji wa mzunguko wa tatu wa Uchambuzi na Tathmini ya Umoja wa Mataifa kuhusu Usafi wa Mazingira na Maji ya Kunywa (GLASS) nchini Nigeria, na aliongoza mpango wa mwaka wa 2020 wa WHO/UNICEF/WSSCC kuunga mkono Mpango wa WASH TRACKFIN ,u uliokuwa na jukumu la kufuatilia uwekezaji na vyanzo vya mapato ya kifedha katika sekta ya serikali ya WASH, kutoka serikali ya Nigeria ,Sekta binafsi na mashirika yasiyo ya Kiserikali ya kimataifa .[7] Mnamo Mei 2019, aliratibu Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha Nigeria (NCDC), Wizara za Shirikisho za Mazingira na umeme, Kazi na Makazi, WHO na washirika wengine katika mpango kwanza wa taifa wa ushirikiano wa sekta mbalimbali wa kukubaliana, kuzuia, na kudhibiti ugonjwa wa Lassa Fever nchini Nigeria.[8][9][10][11]
Machapisho
[hariri | hariri chanzo]Edeh amechapisha kazi kadhaa kuhusu afya ya umma na mazingira ikiwa ni pamoja na kitabu chenye kurasa 426 kinachoitwa “Environmental Health: Understanding Current Issues and Solutions of the 21th Century “ kilichochapishwa mwaka 2016. Kitabu hiki kinatumika kama kitabu cha rejea rasmi katika vyuo vikuu kadhaa barani Africa, ikiwemo Cavendish University-Uganda na Mount Kenya University - Nairobi .[6]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Accolades Pour In For Nigeria's Environmental Health Leader, Isotu-Edeh - News Agency Of Nigeria" (kwa American English). 2023-09-16. Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
- ↑ editor (2022-11-10). "WHO says electronic waste exposure threat to women, children's health - Realnews Magazine" (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
{{cite web}}:|author=has generic name (help) - ↑ editor (2022-11-10). "WHO says electronic waste exposure threat to women, children's health - Realnews Magazine" (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
{{cite web}}:|author=has generic name (help) - ↑ www.premiumtimesng.com https://www.premiumtimesng.com/news/top-news/632498-ncdc-names-four-states-with-highest-cholera-cases.html. Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
{{cite web}}: Missing or empty|title=(help) - ↑ "Edwin Isotu-Edeh | QUICK NEWS AFRICA" (kwa Kiingereza (Uingereza)). 2021-12-22. Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
- 1 2 "Dr. Edwin Edeh(Nigeria)". AFRICAWHOSWHO (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
- ↑ editor (2022-09-07). "Nigeria, WHO, UNICEF, inaugurate hand hygiene roadmap - Realnews Magazine" (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
{{cite web}}:|author=has generic name (help) - ↑ Agency Report (2022-08-27). "Experts Urge Nigerians To prevent Pandemics By Sustaining Ecosystems". Independent Newspaper Nigeria (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
- ↑ csrreporters (2023-09-27). "Sustainability Leaders Laud Edwin Isotu at 40 - Amplifying Africa's Voice for Social Impact and Sustainability" (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
- ↑ Oboh (2022-11-10). "Electronic waste endangers health of mothers, children - WHO". Vanguard News (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.
- ↑ News Agency of Nigeria (2024-02-01). "WHO unveils sanitation safety initiatives in five states". Peoples Gazette Nigeria (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-24.