Dwa (kigoda)
Mandhari

Dwa au asesedwa au wakati mwingine gwa ni kigoda cha Waashanti wa Ghana.
Matumizi
[hariri | hariri chanzo]Mara nyingi hutengenezwa kwa mbao, dwa hupambwa kwa kiwango tofauti kulingana na hadhi ya mwenye kiti hicho,[1] Ina umuhimu mkubwa wa kitaasisi na wa kiishara kati ya watu wa Akan.[2] Viti hivi huwa na umbo la mstatili na vina nguzo tano za kuvinyooshea (annan).[3] Kiti cha kifalme au ahennwa kinachukuliwa kuwa roho ya taifa; mara tu mfalme (ahene) anapokalia kiti hicho, yeye pia huwa mtakatifu kama hicho kiti.[4][5]
Mmarima dwa ni viti vya wanaume, wakati mmaa dwa ni vya wanawake. Adammadwa (ikimaanisha kiti cha senti mbili) ni kwa ajili ya watu maskini.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Christiane Falgayrettes-Leveau, Christiane Owusu-Sarpong, Ghana hier et aujourd'hui, éditions Dapper, 2003
- ↑ Peter Sarpong, The Sacred Stools of the Akan, 1971, p.26
- ↑ Purissima Benitez-Johannot, Jean Paul Barbier-Mueller, Sièges d'Afrique noire du musée Barbier-Mueller, Musée Barbier-Mueller, 2003, p.128
- ↑ Peter Sarpong, The Sacred Stools of the Akan, 1971, p.26
- ↑ Walter C. Rucker, Gold Coast Diasporas : Identity, Culture, and Power, 2015, p.39
| Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Dwa (kigoda) kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |