Dundun oniyeri
Dundun Oniyeri (pia hujulikana kama Yamarita) ni chakula cha Wayoruba kinachotengenezwa kwa viazi vitamu [1] vilivyokaangwa baada ya kufunikwa na mayai.
Viazi vitamu hukatwa vipande vikubwa, kisha hutayarishwa unga wenye viungo pamoja na mayai ya kuchovya.[2] Wakati mwingine unga wa mahindi (cornflour) unaweza kuongezwa, na pia mboga zilizokatwa zinaweza kuchanganywa kwenye mayai. Viazi hivyo huchemshwa kidogo kwanza (parboiled).
Baadaye, vipande vya viazi huchovywa kwenye unga wenye viungo, kisha kwenye mayai yaliyopigwa, na tena kwenye unga. Hatimaye hukaangwa kwenye mafuta ya moto hadi viive vizuri.
Chakula hiki kinaweza kuliwa pekee yake au pamoja na mchuzi wa nyanya na pilipili au mayai.[3] Kinaweza kuliwa kama kitafunwa au mlo kamili.[4]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "How To Make Coated Yam – Yam Burger – Dundun Oniyeri – The online cook" (kwa Kiingereza (Uingereza)). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2026-04-25. Iliwekwa mnamo 2026-04-07.
- ↑ "Yamarita | How to Make Dun Dun Oniyeri". All Nigerian Foods (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2026-04-07.
- ↑ Yetty (2021-01-15). "Recipe How to Make Yamarita and Pepper Sauce". LagosMums (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2026-04-07.
- ↑ Guardian Nigeria (2017-10-30). "Quick Snack: Yamarita Recipe". The Guardian Nigeria News - Nigeria and World News (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2026-04-07.