Ufalme wa Kongo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Dola la Kongo)
Ramani ya kihistoria ya Kongo
Majimbo ya Ufalme wa Kongo mnamo 1648

Ufalme wa Kongo ulikuwa dola la Afrika ya Kati. Eneo lake lilikuwa ndani ya nchi za leo Kongo (Kinshasa), Angola na Kongo (Brazzaville).

Ulianzishwa katika karne ya 14 ikadumu hadi karne ya 17.

Mtawala wake alikuwa na cheo cha "Mwene Kongo" au "Manikongo" wa kabila la Bakongo.

Ufalme huo umejulikana zaidi kihistoria kwa sababu ya mawasiliano yake ya kimataifa. Katika karne ya 15 meli za Wareno zilifika mwambaoni mwake.

Manikongo mbalimbali walijenga uhusiano na Ureno na Kongo ilikuwa taifa la kushikamana na Ureno hadi kuharibika kwa uhusiano huo. Katika kipindi kile taarifa mbalimbali ziliandikwa zinazotupa leo picha nzuri ya ufalme huo.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Wakati wa kukutana na Wareno Ufalme wa Kongo labda ulikuwa na eneo la km² 300,000 ukaunganisha robo ya magharibi ya Kongo (Kinshasa) pamoja na sehemu za Angola na Kongo (Brazzaville).

Utawala[hariri | hariri chanzo]

Manikongo alikaa katika mji wa M'banza-Kongo.

Baada ya wafalme kuwa Wakristo Wakatoliki na kujengwa kwa kanisa kuu, jina la "São Salvador do Congo" (kwa Kireno: "Mwokozi Mtakatifu wa Kongo") lilikuwa kawaida kwa mji mkuu wa milki.

Ufalme ukawa na majimbo, wilaya na vijiji. Majimbo yalikuwa saba ya Mpemba, Nsundi, Mpangu, Mbata, Mbamba na Soyo.

Kwa mikataba ya baadaye falme za Kakongo, Loango na Ngoy likatokea shirikisho ya sehemu nne.