King'amuzi rada

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ditekta ya rada)
King'amuzi Rada
Ditekta ya zamani kidogo.
Ditekta ya Kijapani.

King'amuzi rada (pia: Ditekta ya rada kutoka jina "Radar Detector" kwa lugha ya Kiingereza) ni kifaa cha teknolojia ya juu kinachotambua iwapo mwendo wa gari unafwatiliwa na polisi au walinda sheria wakitumia tochi ya kutambua mwendo (radar gun).

Kifaa hicho cha umeme hutumiwa sanasana na dereva wa gari kuchunguza kama kasi ya magari yao inatazamwa kwa kutumia bunduki ya rada na askari wa usalama wa barabarani au maofisa wengine wa usalama. Wakitambua maeneo ambayo maafisa wa kudhibiti mwendo walipo wanapunguza kasi ya gari kabla ya kusimamishwa na kupewa faini au kutiwa mashakani.

Sheria

Hata hivyo umiliki na matumizi ya King'amuzi rada ni kinyume cha sheria katika nchi nyingi duniani na huchukuliwa kama uvunjaji sheria. Chombo hiki ni kinyume cha sheria kwenye nchi kama vile Australia, Ubelgiji, Brazili na Ufaransa, wakati katika nchi za Japani, Kazakistani, Pakistani na Ufilipino ni halali.

Marekani ni mojawapo kati ya nchi ambako ni kinyume cha sheria kutumia king'amuzi rada bila leseni maalum.[1] Katika baadhi ya nchi, polisi hutumia ditekta ya ditekta ya rada ili kutambua madereva wanaotumia chombo hiki.

Kutumia au kuwa na ditekta ya rada ni kinyume cha sheria katika nchi mbalimbali ambapo ukikutwa nacho unaadhibiwa kwa faini na kunyang'anywa chombo hiki. Nchi hizi huamini kuwa madereva wanaotumia chombo hivi wanahatarisha maisha ya watumiaji wa barabara kuliko madereva wasiotumia.

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.