Delwende
Delwende ni filamu ya drama ya mwaka 2005 ya Burkina Faso iliyoongozwa na S. Pierre Yameogo iliyohusu mama na binti kukataa kufuata mila ya kijinsia ya eneo hilo. Ilionyeshwa katika sehemu ya Un Certain Regard katika Tamasha la Filamu la Cannes la mwaka 2005 ambapo ilishinda katika Tuzo ya Matumaini. [1]
Muktadha
[hariri | hariri chanzo]Baada ya mvulana mdogo kufa kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo, Napoko Diarrha (Yaméogo) anashutumiwa kula nafsi yake kwa sababu ya utamaduni wa kienyeji wa kijinsia.[2]
Wakati hayo yakitokea, mume wake anahisi fedheha kwamba Diarrha anapinga wazo la kumuoza binti yao, hivyo analipiza kisasi kwa kueneza uvumi hatari ambao pengine ungemfanya auawe. Kwa sababu hii, hatima ya Diarrha inaangukia mikononi mwa mzee wa kijiji. Anapojua kwamba atafikishwa Mahakamani, anaamua kukimbilia mji wa karibu zaidi, Ouagadougou, kabla ya hilo kutokea.[2]
Baada ya kufanikiwa kuondoka kijijini kwao, umri wa Diarrha husababisha afya yake kuzorota, huku binti yake akikua.[2]
Muda fulani baadaye, binti yake anaamua kusafiri hadi Ouagadougou, kumtafuta mama yake aliyepotea. Mara tu wanapounganishwa tena, wanajaribu kutoroka kutoka kwa jamii yao inayotawaliwa na wanaume.[2]
Wahusika
[hariri | hariri chanzo]- Blandine Yaméogo kama Napoko
- Claire Ilboudo kama Pougbila
- Célestin Zongo kama Diahra
- Abdoulaye Komboudri kama Nonceur
- Daniel Kabore kama Bancé, Mzee
- Jules Taonssa kama Raogo, Mtabiri
- Thomas Ngourma kama Elie, Mwendawazimu