Daudi Mwangosi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Daudi Mwangosi
Amezaliwa 1972
Busoka mkoani Mbeya.
Amekufa 2 Septemba 2012
kijiji cha Nyololo
Nchi tanzania
Kazi yake mwandishi wa habari wa kituo binafsi cha runinga cha Chanell Ten
Cheo mwenyekiti wa waandishi wa habari Iringa.
Kipindi mwaka 2015
Ndoa ana mke na watoto wanne
Watoto 4
Mahusiano mke


Daudi Mwangosi (1972Septemba 2, 2012) alikuwa mwandishi wa habari wa kituo binafsi cha runinga cha Chanell Ten, Mwangosi aliuliwa katika kijiji cha Nyololo, wilaya ya Mufindi, mkoa wa Iringa ,wakati wa maandamano ya wafuasi wa Chadema.[1][2]

Taaluma[hariri | hariri chanzo]

Daudi Mwangosi alianza kazi ya uandishi wa habari mnamo mwaka 2015 katika kituo cha runinga cha Chanell ten ambacho ni kituo cha habari binafsi na mnamo mwaka 2011 alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa waandishi wa habari Iringa.

Kifo[hariri | hariri chanzo]

Nyololo iko nje ya Iringa, Tanzania. Inaonyeshwa hapa kuhusiana na mji mkuu wa Dodoma.

Mnamo 2 Septemba 2012, Daudi Mwangosi aliuliwa katika kijiji cha Nyololo wakati akifuatilia ufunguzi wa ofisi ya Chadema, chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania. Mwangosi alikuwa akifuatilia tukio la ufunguzi huo na wakati huo polisi walikuwa wamezuia mkusanyiko wa wafuasi wa chama hicho cha siasa kwa sababu ilidaiwa kuwa kinyume cha sheria.[3], Mwangosi aliuliwa kwa kupigwa bomu wakati akijaribu kumsaidia muandishi mwenzake Godfrey Mushi alokuwa muandishi wa gazeti la Nipashe .[4][2][5]

Mwangosi aliaga dunia baada ya kupigwa [bomu la machozi] tumboni kwa karibu zaidi na kusababisha mauti yake, askari alohusika na mauaji yake alihukumiwa kifungo cha miaka kumi na tano gerezani.

Mwangosi aliaga dunia akiwa na umri wa miaka arobaini, aliacha mke na watoto wanne.[6], alizikwa katika kijiji cha Busoka mkoani Mbeya.[7][5]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Tanzanian TV journalist killed", September 3, 2012. 
  2. 2.0 2.1 "Prominent Tanzanian journalist killed in scuffle with police". Committee to Protect Journalists. September 4, 2012.  Check date values in: |date= (help)
  3. "Team to investigate killing of Dar TV reporter - News". nation.co.ke. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-09-06. Iliwekwa mnamo 2013-10-05. 
  4. Ng, Fumbuka (September 4, 2012). "Tanzanian journalist killed reporting police-opposition clash". Reuters. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2014-03-18. Iliwekwa mnamo April 22, 2017.  Unknown parameter |= ignored (help); Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  5. 5.0 5.1 "Prominent Tanzanian journalist killed in scuffle with police -". Committee to Protect Journalists. 2012-09-04. Iliwekwa mnamo 2013-10-05. 
  6. "Daudi Mwangosi". Committee to Protect Journalists. September 2, 2012.  Check date values in: |date= (help)
  7. UjenziOnline. "MWANDISHI DAUDI MWANGOSI AZIKWA KIJIJINI KWAKE...". 
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Daudi Mwangosi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.