Nenda kwa yaliyomo

Cyril Stober

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Cyril Stober ni mwandishi wa habari na mtangazaji kutoka nchini Nigeria. [1] Alizaliwa katika Jimbo la Niger. Alisoma katika Shule ya Sekondari ya Fatima ambayo sasa inajulikana kama Father O'Connell Science College, Minna.

Stober alitumia zaidi ya miongo mitatu ya maisha yake ya kazi kama mtangazaji wa habari na mwanahabari. Jukumu lake kuu lilikuwa ni kuendesha taarifa ya habari ya saa 3 usiku katika mtandao wa NTA na taarifa ya habari ya NTA Prime Time. Mavazi yake ya kutambulisha yalikuwa ni vazi la kienyeji, kofia na miwani yake. Mwaka 2015, kulikuwa na uvumi kwamba alikuwa amestaafu, lakini aliwashangaza watazamaji alipoonekana tena akiendesha taarifa ya habari.[2] Tarehe 21 Aprili 2019, Stober alistaafu Mamlaka ya Utangazaji ya Nigeria. Cyril Stober bado anaendesha vipindi vya kawaida vya mtandao wa NTA baada ya kustaafu kwani anachukuliwa kama mfano wa kuigwa kwa Nigeria. [3] [4] [5]

  1. Verity (10 Desemba 2015). "As Cyril Stober Takes A Bow, Here Are 6 Facts You Should Know About Him". Information Nigeria. Iliwekwa mnamo 14 Mei 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. Temitope Alabi (2019-04-21). "Veteran NTA News Bfoadcaster, Cyril Stober retires". Information Nigeria (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-15.
  3. "Nigerian Twitter reacts to Cyril Stober's retirement from broadcasting". guardian.ng. Iliwekwa mnamo 14 Mei 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. Durojaiye, Seun (23 Aprili 2019). "Nigerians react as veteran NTA newscaster Cyril Stober retires". Legit.ng – Nigeria news. Iliwekwa mnamo 14 Mei 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. emmanuel (22 Aprili 2019). "Twitter Standing Ovation as Cyril Stober Retires from NTA". Olisa.tv. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-05-14. Iliwekwa mnamo 14 Mei 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)