Nenda kwa yaliyomo

Constantine Koronin

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Constantine Coronini)

Constantine Koronin (Gorodishche, Wilaya ya Solikamsky, 19 Septemba 1881 - Harbin, China, 11 Desemba 1924) alikuwa padri wa Kanisa la Kiorthodoksi la Urusi, baadaye wa Kanisa Katoliki la Kigiriki.

Alizaliwa katika dayosisi ya Kiorthodoksi ya Perm, akiwa mwana wa John Koronin. Koronin alisoma katika Seminari ya Theolojia ya Perm na ile ya Tiflis, na mwaka 1909 alihitimu kutoka Chuo cha Theolojia cha Saint Petersburg akiwa na shahada ya theolojia. Pia alisoma katika Taasisi ya Kiimla ya Akiolojia.

Constantine Koronin alihudumu kama paroko wa kanisa katika wilaya ya Petrakovskaya (Dayosisi ya Warsaw), na tangu mwaka 1913 alikuwa paroko katika gereza la Warsaw. Kuanzia mwanzo wa Vita ya Kwanza ya Dunia, alihamishwa. Mnamo mwaka 1915, aliteuliwa kuwa paroko wa Kanisa Kuu la Chita, mjumbe wa Baraza la Dayosisi la Trans-Baikal, na mhubiri wa kimisheni wa dayosisi hiyo.

Mnamo mwaka 1921, alinusurika majaribio mawili ya kuuawa yaliyofanywa na Wabolsheviki, na mwaka huohuo alihamia nchini China, ambako alikuWa abati wa Kanisa Takatifu la Iver mjini Harbin, profesa wa Taasisi ya Kipolitechiki ya Urusi-China, na mwenyekiti wa kamati iliyotayarisha Baraza la Makanisa ya Mashariki ya Mbali.

Mnamo mwaka 1923, Koronin alijiunga na Kanisa Katoliki baada ya kutoka katika Ukristo wa Kiorthodoksi wa Urusi, na alifariki dunia mwaka 1924 kutokana na saratani ya tumbo.[1]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.