Nenda kwa yaliyomo

Clinton N'Jie

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Clinton Mua N'Jie (alizaliwa 15 Agosti 1993) ni mchezaji wa soka kutoka Kamerun anayecheza kama mshambuliaji.

N'Jie alianza taaluma yake katika Olympique Lyonnais (Lyon), akipanda kutoka programu ya vijana hadi kikosi cha B, kisha kujiunga na kikosi cha kwanza kinachoshiriki Ligue 1 ya Ufaransa. Baadaye alisajiliwa na Tottenham Hotspur ya Ligu Kuu ya Uingereza EPL, kabla ya kurejea Ufaransa kujiunga na Olympique de Marseille.

Baadaye aliendelea kucheza katika vilabu vingine nje ya Ulaya, ikiwa ni pamoja na CSKA Moscow na Sivasspor.[1]

Kwa upande wa timu ya taifa, N'Jie alicheza mechi yake ya kwanza kwa Cameroon mwaka 2014. Ameshiriki katika Africa Cup of Nations za 2015, 2017, 2019, na 2021, akishinda taji la mwaka 2017 na kufikia nafasi ya tatu mwaka 2021.[2]

  1. "Tottenham transfer news: Cameroon striker close to securing £10m switch to White Hart Lane". talkSPORT. 12 Agosti 2015. Iliwekwa mnamo 13 Agosti 2015.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "Clinton N'Jie extends Lyon contract and scores his first goal". BBC Sport. BBC Sport. 24 Septemba 2014. Iliwekwa mnamo 13 Agosti 2015.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Clinton N'Jie kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.