Nenda kwa yaliyomo

Charles II wa Uingereza

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Taswira ya Charles II wa Uingereza

Charles II (29 Mei 1630 – 6 Februari 1685) alikuwa mfalme wa Uingereza, Ireland, na Uskoti kuanzia mwaka 1649 hadi 1685. Baba yake alikuwa Charles I, ambaye aliuawa baada ya kushindwa kwenye vita dhidi ya Bunge.

Maisha ya awali

[hariri | hariri chanzo]

Charles alikuwa mtoto wa kwanza wa mfalme. Akiwa mtoto mdogo, alipewa cheo cha Mwanamfalme wa Wales kama ishara ya kwamba atakuja kurithi ufalme.

Alipofikia ujana, baba yake tayari alikuwa vitani na Bunge katika Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Uingereza.

Mwanamfalme Charles hakushiriki sana katika mapigano. Mama yake, Henrietta Maria, alikuwa Mfaransa, na alimpeleka pamoja na ndugu zake Ufaransa wakati vita vilipoanza ili kuwaweka salama.

Alipokuwa na umri wa miaka kumi na minane, alipokea habari kwamba baba yake ameuawa.

Hili lilimfanya kuwa mfalme, akaanza kujiita Charles II mara moja. Hata hivyo, Bunge lilikuwa bado linadhibiti Uingereza na halikumruhusu kuchukua kiti cha enzi kwa sababu baada ya kuuawa kwa Charles I, Oliver Cromwell alichukua madaraka kama Lord Protector wa Uingereza kutoka mwaka 1653 hadi 1658.

Kukimbia kwa Mfalme

[hariri | hariri chanzo]

Mnamo 1651, Charles II alirudi Uingereza na kupambana na Bunge katika Mapigano ya Worcester.

Alishindwa, lakini inasemekana alitoroka kwa kujificha kwenye mti wa mwaloni.

Baadaye, alilazimika kujifanya mtumishi. Binti mmoja aitwaye Jane Lane alimsaidia kutoroka, akaelekea Uholanzi kuungana tena na wafuasi wake. Alikaa huko hadi mwaka 1660.

Marejeo ya Ufalme

[hariri | hariri chanzo]

Wakati Charles II akiwa Uholanzi, Uingereza ilikuwa inatawaliwa na Oliver Cromwell, ambaye alikuwa kiongozi wa nchi kwa uamuzi wa Bunge. Baada ya Cromwell kufariki mwaka 1658, mwanawe Richard Cromwell alichaguliwa kuchukua madaraka.

Hata hivyo, Richard Cromwell hakuwa na uwezo wa uongozi kama baba yake. Hii ilipelekea Charles II kuitwa arudi kutawala Uingereza. Mnamo 1660, Charles II alirejea Uingereza na kuchukua kiti cha enzi. Tukio hili linajulikana kama Kurudi kwa Uingereza.

Baadhi ya maadui wake walihukumiwa kwa kumwua baba yake na kumpinga yeye, lakini Richard Cromwell aliruhusiwa kuishi maisha ya kawaida nje ya London.

Charles II alikuwa maarufu na alijulikana kama "Mfalme Mwenye Furaha" kwa sababu alifuta sheria nyingi ambazo Cromwell alikuwa ameweka akaruhusu hivyo watu kuwa na uhuru wa kufurahia maisha yao.

Alipenda kwenda kwenye maonyesho ya michezo ya kuigiza, kucheza karata, na kushiriki katika michezo kama vile mbio za farasi.

Baadhi ya watu waliona kwamba mfalme alipaswa kuwa mtu makini na asitumie muda mwingi na pesa kwa starehe.

Kulikuwa pia na wale waliompinga kwa sababu ya imani yake ya kidini. Alilelewa na mama yake, ambaye alikuwa Mkatoliki, ilhali watu wengi nchini walikuwa Waprotestanti.

Alioa mrembo kutoka Ureno, Catherine wa Braganza. Hawakupata watoto, lakini Charles alikataa kuachana naye. Kabla ya ndoa yake, alikuwa na wapenzi wengi, na hata baada ya kuoa aliendelea kuwa na masuria.

Mmoja wa hao masuria maarufu alikuwa mwigizaji aitwaye Nell Gwyn. Baadhi ya masuria wake walizaa watoto naye. Hata hivyo, hakuna hata mmoja aliyeruhusiwa kuwa mfalme kwa sababu walikuwa watoto wa nje ya ndoa.

Mtoto maarufu zaidi wa Charles II alikuwa James Scott. Charles alimpa cheo cha Duke wa Monmouth. Mama yake James alikuwa mpenzi wa Charles wakati alipokuwa Uholanzi, na baadhi ya watu walidai walifunga ndoa kwa siri. Kama hilo lingekuwa kweli, basi James angeweza kuwa mfalme baada ya kifo cha Charles II. Watu wengi walitaka hili litokee kwa sababu hawakupenda wazo la kaka yake Charles, aitwaye James, kuwa mfalme. James alikuwa Mkatoliki, jambo ambalo lilimfanya asipendwe sana.

Charles II alifariki ghafla kutokana na ugonjwa, na mwanawe Duke wa Monmouth alianzisha uasi kwa matumaini ya kuwa mfalme. Hata hivyo, alishindwa na jeshi la kifalme, ambalo lilimuunga mkono kaka yake Charles II. Duke wa Monmouth alihukumiwa kifo kwa kukatwa kichwa, na kaka yake Charles, James II wa Uingereza, akawa mfalme mpya.

Alimotajwa

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]