Chama cha Kidemokrasia cha Marekani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Chama cha Kidemokrasia cha Marekani (Kiing. “Democratic Party”) ni chama cha kisiasa nchini Marekani. Kilianzishwa mwaka wa 1828 na Rais Andrew Jackson, yaani ni chama cha zamani kabisa duniani ambacho bado hufanya kazi. Kikawa chama chenye nguvu tangu pale kikishindana na Chama cha Jamhuri. Kulikuwa na Marais kumi na wanne kutoka Chama cha Kidemokrasia, kuanzia Andrew Jackson (1829-1837) hadi Barack Obama (2009-2017).