Chaïbia Talal
Chaïbia Talal (Kiarabu: الشعيبية طلال; a 1929 - 2 Aprili 2004) alikuwa mchoraji wa Moroko. [1]
Wasifu
[hariri | hariri chanzo]| Chaïbia Talal | |
| Amezaliwa | 1929 |
|---|---|
| Amekufa | 2/4/2024 Casablanca, Morocco |
| Nchi | Moroko |
| Kazi yake | Mchoraji wa picha |
Chaïbia alizaliwa Chtouka, kijiji kidogo karibu na El Jadida, nchini Morocco mwaka 1929.Akiwa na umri wa miaka 13, alitumwa Casablanca na wazazi wake ili kuolewa na mwanaume mwenye umri wa miaka 70. Alipofikisha umri wa miaka 14, alikuwa tayari amejifungua mtoto wa kiume aliyeitwa Hocein, na alipofikisha miaka 15 alibaki mjane. Baada ya kifo cha mume wake, alifanya kazi ya usaidizi wa nyumbani (mfanyakazi wa ndani) ili kupata kipato cha kumtunza yeye mwenyewe na mwanawe.[2] Talal alikuwa na dhamira kubwa ya kuhakikisha mwanawe anapata elimu, hususan elimu ya kitaaluma na ujuzi wa kusoma na kuandika, ingawa yeye mwenyewe Talal alibaki hajui kusoma wala kuandika maisha yake yote. Baada ya kuota ndoto ambayo alipokea vifaa vya kuchorea kutoka kwa watu wasiojulikana, alipata msukumo wa kuanza kuchora.[3]
Kazi zake hazikupokelewa vizuri mwanzoni katika ulimwengu wa sanaa wa Morocco. Mwana wa Talal alikuja kuwa msanii anayeheshimika kwa haki yake mwenyewe, na mwaka 1965 alimfahamisha Talal kwa mkurugenzi wa Makumbusho ya Sanaa ya Kisasa ya Paris, Pierre Gaudibert, ambaye alivutiwa sana na kazi zake. Kufuatia mkutano huo, kazi zake zilionyeshwa katika Taasisi ya Goethe mjini Casablanca na katika Makumbusho ya Sanaa ya Kisasa ya Paris mwaka 1966.[4]
Kwa kuwa alikuwa msanii aliyejifunza mwenyewe bila mafunzo rasmi, Talal alijulikana kwa kuvunja mipaka ya mila za jadi za sanaa.[5] Kazi zake zimeainishwa kama “sanaa ya nje” (outsider art),, aina ya sanaa inayoonesha mawazo yasiyo ya kawaida kutoka kwa watu walioko nje ya mikondo ya sanaa ya kawaida Aliathiriwa na kazi za wasanii wa harakati ya uchoraji ya CoBrA. Kazi zake pia huchukuliwa na baadhi ya watu, akiwemo mwandishi wa habari Ahmed El Fassi, kuwa niza sanaa ya kiasili/rahisi (naïve art) ya kiasili/rahisi (naïve art.
Mwaka 2015, mtayarishaji wa filamu wa Morocco, Youssef Britel, alitengenChaïbia.mFilamuasifu iliyopewa jina Chaïbia. Filamu hiyo iliandikwa na David Villemin na Youssef Britel, na ilimshirikisha Saadia Azn katika2004asi ya Chaïbia Talal.[6]
Mwaka 2004, Talal alifariki dunia kutokana na mshtuko wa moyo huko Cblanca akiwa na umri wa miaka 75.
Kazi za Talal zinaendelea kuonyeshwa hadi leo, ikiwemo katikaMwaka wa Utamaduni Qatar–Morocco 2024, ambapo kazi zake zilijumuishwa katika sehemu iliyohusu , ambapo kazi zake zilijumuishwa katika sehemu iliyohusu Wanawake katika Jamii.[7]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Cinéma: Chaïbia, La Paysanne des Arts, en salles le 16 décembre" [Cinema: Chaïbia, La Paysanne des Arts, in theaters on December 16]. 1 Desemba 2015.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "L'artiste peintre Chaibia au cinéma", Al HuffPost Maghreb (kwa Kifaransa), 2015-02-25, iliwekwa mnamo 2026-01-11
- ↑ LE MATIN (2004-04-03). "Chaïbia portée en terre : les couleurs du terroir en deuil". Le Matin.ma (kwa Kifaransa). Iliwekwa mnamo 2026-01-11.
- ↑ "Chaïbia Talal". Obelisk Art History (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2026-01-11.
- ↑ kristen-gianaris (2020-05-30). "Chaibia Talal, Morocco's Most Famed 20th Century Painter". Morocco World News (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2026-01-11.
- ↑ Chaïbia (2015) ⭐ 6.8 | Biography (kwa American English), iliwekwa mnamo 2026-01-11
- ↑ The Peninsula Newspaper (2024-03-19). "Museums in Qatar highlight Moroccan culture, artistry". thepeninsulaqatar.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2026-01-11.
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Chaïbia Talal kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |