Nenda kwa yaliyomo

Cartagena, Kolombia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Cartagena inayojulikana tangu enzi za kifalme kama Cartagena de Indias, ni mji na moja ya bandari kuu kwenye pwani ya kaskazini ya Kolombia katika Kanda ya Pwani ya Karibi, kando ya Bahari ya Karibi. Jukumu la zamani la mji huu kama kiungo cha kuelekea West Indies unalipa thamani kubwa ya kihistoria kwa ugunduzi wa dunia na uhifadhi wa urithi wa njia kuu za biashara ya baharini.[1] Kama koloni la zamani la Hispania, ulikuwa mji wa bandari muhimu kwa mauzo ya fedha ya Bolivia kwenda Uhispania na uingizaji wa Waafrika waliofanywa watumwa.[2] Eneo lake la kimkakati lilifanya uwe bandari kuu ya biashara ya kifalme na ukaanzisha umuhimu wake mwanzoni mwa miaka ya 1540.

Cartagena ya sasa ni mji mkuu wa Bolívar Department, na ulikuwa na idadi ya watu 876,885 kulingana na sensa ya 2018,[3] na kuufanya kuwa mji wa pili kwa ukubwa katika kanda ya Karibi, baada ya Barranquilla, na mji wa tano kwa ukubwa nchini Kolombia. Shughuli za kiuchumi ni pamoja na viwanda vya baharini na kikemikali, pamoja na utalii.

Kihistoria, mji huu ulianzishwa mnamo tarehe 1 Juni 1533, na kuufanya kuwa mmoja wa miji ya zamani zaidi ya kikoloni huko Amerika Kusini;[4] lakini makazi ya wenyeji asili katika eneo hilo yalianza tangu mwaka 4000 KK. Wakati wa ukoloni wa Uhispania, Cartagena ilikuwa na jukumu kuu katika utawala na upanuzi wa Dola la Uhispania. Mnamo mwaka 1984, mji wa kikoloni uliozungushwa ukuta na ngome za Cartagena ulitangazwa kuwa UNESCO World Heritage Site. Pia, ulikuwa uwanja wa Mapigano ya Cartagena de Indias mnamo 1741 kati ya Uhispania na Uingereza.

Mabaki ya nyumba za wenyeji wa zamani wa mji huu

Utamaduni wa Puerto Hormiga, ulioanzishwa katika eneo la pwani ya Karibi, unaonekana kuwa jamii ya kwanza ya wanadamu iliyofanyiwa utafiti katika eneo ambalo sasa ni Kolombia.[5] Wanaakiolojia wanakadiria kuwa karibu mwaka 4000 KK, utamaduni huu ulipatikana karibu na mipaka ya sasa ya Bolívar na Sucre, ambapo waligundua vitu vya kauri vya zamani zaidi huko Amerika.[6]

Baada ya kuporomoka kwa utamaduni huu karibu mwaka 3000 KK, utamaduni ulioendelea zaidi wa Monsú uliibuka karibu na vitongoji vya sasa vya Cartagena, ukichanganya uchumi vya kilimo na uvuvi.[7] Hatimaye, jamii ya Sinú ilitawala eneo hilo. Hadi ukoloni wa Uhispania, makabila mbalimbali ya lugha za Karib, Malibu, na Arawak yalishi kando ya pwani. Karibu mwaka 1500 BK, eneo hilo lilikaliwa na makabila tofauti ya familia ya lugha ya Karibi, hasa jamii ndogo ya Mocanae, ikiwa ni pamoja na kabila la Kalamarí ambalo lilikuwa na nguvu zaidi katika eneo la mji wa sasa.[8] Makabila haya yalishiriki usanifu wa pamoja wa vibanda vya mbao vilivyozungushwa kuta za kujihami.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. Centre, UNESCO World Heritage. "Port, Fortresses and Group of Monuments, Cartagena". UNESCO World Heritage Centre (kwa Kiingereza).
  2. Lance R. Grahn, "Cartagena" in Encyclopedia of Latin American History and Culture, vol. 1, p 581. New York: Charles Scribner's Sons 1996.
  3. Citypopulation.de
  4. "Big on Charm: Colonial Cartagena". Travel (kwa Kiingereza). 17 Novemba 2015.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. Carvajal Contreras, Diana Rocío; Iizuka, Fumie. "Un análisis visual de técnicas de manufactura y tecnología de la cerámica del sitio Puerto Hormiga, Colombia". Arqueología y Patrimonio.
  6. "Biblioteca Luis Ángel Arango". Lablaa.org. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 23 Septemba 2006. Iliwekwa mnamo 26 Machi 2013.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  7. "Biblioteca Luis Ángel Arango". Lablaa.org. 4 Juni 2005. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 1 Desemba 2008. Iliwekwa mnamo 24 Juni 2010.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  8. Lemaitre, Eduardo (1994). A Brief History of Cartagena. Medellin: Compania Litografica Nacional S.A. uk. 13. ISBN 978-958-638-092-8.