Nenda kwa yaliyomo

Carol Rymer Davis

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Carol Ann Rymer Davis (28 Novemba 194429 Septemba 2010) alikuwa Mmarekani mpandaji puto la anga na mtaalamu wa radiolojia. Mnamo 2004, alikuwa mwanamke wa kwanza kushinda Kombe la Gordon Bennet katika mashindano ya puto la anga pamoja na mwenzake Richard Abruzzo. Kwa ushindi huu wa kihistoria, walitunukiwa Harmon Trophy ya mwaka 2005. Alipotea baharini mnamo 29 Septemba, 2010, juu ya Bahari ya Adriatic. Mwili wake, pamoja na ule wa Abruzzo, ulipatikana pwani ya Italia katika Bahari ya Adriatic mnamo 6 Desemba, 2010.[1]

Maisha ya awali na elimu

[hariri | hariri chanzo]

Rymer Davis alizaliwa huko Denver, Colorado mnamo 28 Novemba 1944, akiwa binti wa madaktari Charles na Marion Rymer. Alihitimu kutoka Chuo cha Colorado akiwa na shahada ya kwanza, na katika Chuo Kikuu cha Colorado Boulder, Health Sciences Center akiwa na shahada ya udaktari wa tiba. Alikamilisha mafunzo yake ya udaktari bingwa (residency) huko Albuquerque katika Kituo cha Tiba cha Lovelace.

Alihudumu kwa miaka 22 katika Jeshi la Akiba la Marekani kama daktari wa ndege na kustaafu akiwa na cheo cha kanali mwaka 2001. Alipokea Medali ya Huduma ya Kipekee na alikuwa Mhitimu Bora katika Shule ya Expert Field Medical Badge huko Fort Carson.

  1. [(http://news.sky.com/skynews/Article/201012115848431) Bodies Of Missing Balloonists Found In Sea] – Sky News
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Carol Rymer Davis kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.