Nenda kwa yaliyomo

Carlo Acutis

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Masalia za nywele za Carlo Acutis, yakionyeshwa katika kikanisa cha Katerina wa Aleksandria, ndani ya kanisa la Mt. Fransisko huko Lodi, Italia.

Carlo Acutis (London, Uingereza [1], 3 Mei 1991Monza, Italia, 12 Oktoba 2006) alikuwa mvulana ambaye alijulikana kwa uchangamfu wake, ustadi wa kutumia kompyuta, na kujitolea kwa masuala yahusuyo Ekaristi, ambayo ilikuwa mada kuu ya maisha yake. Aliandika juu ya miujiza iliyohusiana na Ekaristi takatifu na matokeo ya Bikira Maria duniani yaliyoidhinishwa, na kuyapanga mambo hayo yote kwenye tovuti aliyoibuni kabla ya kifo chake kilichotokana na saratani ya damu.

Alitangazwa mwenye heri na Papa Fransisko tarehe 10 Oktoba 2020. Baada ya muujiza wa pili unaohusishwa na maombezi ya Acutis kuthibitishwa mnamo Mei 2024, Papa huyo alitoa kibali mnamo Julai 2024 ili atangazwe mtakatifu tarehe 27 Aprili 2025, ila mwenyewe alifariki kabla ya tarehe hiyo, hivyo tukio liliahirishwa. [2] Hatimaye Papa Leo XIV alimtangaza tarehe 7 Septemba 2025.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. Syed, Armani (2024-05-24). "British-Born Teenager Set to Become First Millennial Saint". TIME (kwa Kiingereza). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2024-09-01. Iliwekwa mnamo 2024-11-04.
  2. Mares, Courtney (20 Nov 2024). "Pope Francis announces 2025 canonizations for Carlo Acutis, Pier Giorgio Frassati during Jubilee celebrations". Catholic News Agency.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.