Candice Boucher
Mandhari
Candice Boucher ni mwanamitindo na mwigizaji kutoka nchini Afrika Kusini. Mnamo mwaka 2010, Boucher alionekana kwenye jalada la majarida ya Playboy na Sports Illustrated. Mwaka 2011, aliigiza katika filamu ya Bollywood iitwayo Aazaan.
Candice Boucher alizaliwa mjini Durban, Afrika Kusini. Akiwa na umri wa miaka kumi na saba, alishiriki katika shindano la kila mwaka la urembo la shule yake ya sekondari kwa ushawishi wa marafiki zake.
Alishinda shindano hilo pamoja na kupiga picha za kitaaluma na mpiga picha wa eneo hilo. Mpiga picha huyo alituma picha za Boucher kwa wakala wa uanamitindo wa Afrika Kusini unaoitwa Models International. Kampuni hiyo ilimtafuta Boucher na kumpa uwakilishi rasmi wa uanamitindo.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Local model in Playboy". iAfrica. 5 Septemba 2013. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 5 Septemba 2013. Iliwekwa mnamo 13 Januari 2020.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Candice Boucher kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |