Bien-Aimé Baraza
Bien-Aimé Alusa Baraza (anajulikana kama Bien; amezaliwa Nairobi, 28 Desemba 1987) ni mwimbaji, mtunzi wa nyimbo, na mpiga gitaa kutoka Kenya, mwanachama wa bendi maarufu ya muziki wa Afropop iitwayo Sauti Sol.
Kama msanii wa kujitegemea, Bien amepata mafanikio ya kibiashara na albamu yake ya kwanza Alusa Why Are You Topless? na ni mwanzilishi mwenza wa lebo ya muziki Sol Generation Records. Yeye pia ni mtunzi wa nyimbo aliyeidhinishwa na Grammy kwa mchango wake katika albamu ya Burna Boy Twice as Tall.[1]
Maisha ya awali na elimu
[hariri | hariri chanzo]Bien-Aimé Alusa Baraza alizaliwa na kulelewa Nairobi, Kenya. Alisoma katika Shule ya Upper Hill, ambako alikutana na wanabendi wenzake wa baadaye wa Sauti Sol, Willis Chimano na Savara Mudigi. Kundi hilo lilianza kama kundi la kuimba cappella liitwalo Voices in the Light.[2]Mwanachama wa nne, mpiga gitaa Polycarp Otieno, alijiunga nao baada ya wao kuhitimu.
Baada ya kumaliza shule ya upili, Bien alijiunga na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Merika cha Afrika (USIU-Afrika), ambako alihitimu mwaka wa 2011 na Shahada ya Sanaa katika Uandishi wa Habari na Mafunzo ya Vyombo vya Habari.[3]
Kazi
[hariri | hariri chanzo]Sauti Sol
[hariri | hariri chanzo]Kama mwimbaji mkuu na mtunzi wa nyimbo za Sauti Sol, Bien alikuwa kiini cha kuinuka kwa bendi na kuwa mojawapo ya vikundi vya muziki vilivyofanikiwa zaidi barani Afrika. Bendi hiyo ilianzishwa mwaka wa 2005, na ikapata umaarufu wa kimataifa kutokana na sauti yake ya kipekee, ambayo ilichanganya mitindo ya jadi ya muziki wa Kenya na muziki wa kisasa waAfropop na R&B. Bendi hiyo imetoa albamu kadhaa zilizopokelewa vizuri na wakosoaji wa muziki sana, zikiwemo Mwanzo (2008), Sol Filosofia (2011), Live and Die in Afrika (2015), Afrikan Sauce (2019), na Midnight Train (2020).
Mnamo Mei 2023, Sauti Sol walitangaza kuwa "watapumzika kwa muda usiojulikana" baada ya kumaliza ziara yao ya mwisho ya dunia, ili kuwapa nafasi wanachama wake kujikita katika miradi yao binafsi ya muziki.
Kazi ya pekee
[hariri | hariri chanzo]Bien amekuwa akijihusisha na miradi ya kibinafsi kwa miaka kadhaa, lakini rasmi,taaluma yake ya muziki wa kujitegemea ilishika kasi mwaka wa 2021. Alisaini mkataba na Sol Generation Records, lebo ya muziki aliyoanzisha pamoja na wenzake ili kutoa miradi yake ya kibinafsi.[4]
Mwezi Novemba 2021, Bien alitoa EP yake ya kwanza, Bald Men Love Better,ambayo ilikuwa ushirikiano na mpiga pianowa muziki wa jazz Aaron Rimbui . EP hiyo ilisifiwa kwa ubora wake wa kimuziki na maneno yake ya ndani yenye tafakari ya kina.[5]
Mnamo Novemba 2023, Bien alitoa albamu yake ya kwanza ya urefu kamili, Alusa Why Are You Topless? Albamu hiyo yenye nyimbo 16 ilijumuisha ushirikiano na wasanii wa kimataifa, wakiwemo Ayra Starr, Ms Banks, na Scar Mkadinali.[6]Mwezi huo huo, alikua msanii wa nne kutoka Kenya kushirikishwa kwenye jukwaa maarufu la muziki la Ujerumani COLORSxSTUDIOS, ambapo aliimba wimbo wake "True Love."[7]
Alianza ziara yake ya Ulaya mapema mwaka wa 2024 kwa ajili ya kukuza albamu hiyo.[8] Mwezi Julai 2024, alitoa toleo la kisasa la albamu, lililojumuisha nyimbo mpya na ushirikiano na wasanii kama Fally Ipupa na Adekunle Gold.[9]Muziki wake umefanikiwa sana ya kibiashara; mwaka wa 2024, Spotify ilimtaja kuwa msanii wa Kenya aliyesikilizwa zaidi mwaka huo.[10]
Usanii na uanaharakati
[hariri | hariri chanzo]Muziki wa Bien unachanganya mitindo ya Afropop na vipengele vya Rhumba, R&B, na Afrobeats . Uandishi wake wa nyimbo mara nyingi huzingatia mada za mapenzi, uhusiano, na maoni ya kijamii. Nyimbo kama vile "Maandamano", aliyoimba kwa ushirikiano na rapa Breeder LW, inazungumzia moja kwa moja maswala ya kisiasa na kijamii yanayoathiri Wakenya.[11]
Yeye ni mtetezi mashuhuri wa haki za wasanii na mara kwa mara amekuwa amekosoa Music Copyright Society of Kenya (MCSK) kwa kile anachotaja kuwa malipo duni ya mirabaha kwa wanamuziki.[12]Pia ameonyesha waziwazi hadharani kuunga mkono haki za LGBTQ+ nchini Kenya.[13]
Miradi mingine
[hariri | hariri chanzo]Pamoja na wanabendi wenzake wa Sauti Sol, Bien ni mwanzilishi mwenza na mkurugenzi wa miradi kadhaa ya kibiashara:
- Sol Generation Records : Lebo ya huduma kamili ya rekodi na kampuni ya sanaa ya ubunifu.
- Hustle Sasa : Jukwaa la kidijitali za biashara linalowawezesha wabunifu kuuza bidhaa moja kwa moja kwa hadhira yao.[14]
- Sol Kids : Kampuni inayojikita katika kutengeneza maudhui kwa ajili ya watoto, ikiwa ni pamoja na vitabu na vibonzo.
Mwaka 2022, Bien alifungua klabu ya usiku jijini Nairobi iitwayo The Manhattan Ke Bar and Grill.[15]Pia anahudumu katika bodi ya Recording Industry of Kenya (RIKE).[16]
Maisha binafsi
[hariri | hariri chanzo]Mnamo Machi 2020, Bien alifunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu, Chiki Kuruka, ambaye ni mwalimu wa mazoezi ya mwili na mtunzi wa media, na pia anahudumu kama meneja wake.[17]
Tuzo na kutambuliwa
[hariri | hariri chanzo]Kama mwanachama wa Sauti Sol, Bien ameshinda tuzo nyingi, zikiwemo Tuzo za Muziki za MTV Europe na tuzo nyingi za AFRIMA .Zifuatazo ni tuzo alizopokea kutokana na kazi yake kama mtunzi wa nyimbo na msanii wa kujitegemea
| Mwaka | Sherehe ya Tuzo | Kategoria | Kazi | Matokeo | Kumb. |
|---|---|---|---|---|---|
| 2021 | 63rd Grammy Awards | Best Global Music Album | Twice as Tall(as songwriter | Won | [1] |
| 2024 | Basata Music Awards (Tanzania) | Best African Song | "Komasava"(with Mbosso) | Won | [18] |
| Pulse Music Video Awards(Kenya) | Male Video Of the Year | "My Baby" | Won | [19] | |
| 2025 | Trace Awards | Best Artist-East Africa | Himself | Won | [20] |
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- 1 2 Njeri (2021-03-17). "Bien, Bensoul Named Grammy Award-Winning Songwriters". KenyanVibe (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Bien lands in Paris as his much-anticipated Europe tour kicks off". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2024-03-07. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Sauti Sol's Bien: Music paid my entire university fees". Nairobi News (kwa American English). 2023-03-13. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Bien signs Ksh.50 million deal with Sol Generation, a record label he helped found". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2021-11-05. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ Charles Maganga (2021-11-05). "Bien Releases 'Bald Men Love Better' EP Featuring Aaron Rimbui". NotjustOk (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "'Alusa Why Are You Topless?' Bien finally drops debut solo album". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2023-11-17. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Sauti Sol's Bien becomes fourth Kenyan artiste to be featured on COLORS Studios". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2023-11-07. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Bien lands in Paris as his much-anticipated Europe tour kicks off". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2024-03-07. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Sauti Sol's Bien ventures into business, opens new pub". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2022-08-02. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ Sophie Opondo (2024-12-09). "Bien dethrones Wakadinali as Spotify's Top Kenyan Artist of 2024". TV47 Digital (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Beyond beats: Why Bien's voice will always echo in your mind | Pulselive Kenya". www.pulselive.co.ke (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Why I turned down MCSK invite to collect my royalties - Bien". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2024-02-29. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Songaplay". songaplay.com. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Musician's app helps Kenyan creatives sell music and merchandise". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2023-01-04. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "Sauti Sol's Bien ventures into business, opens new pub". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2022-08-02. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "RIKE, new association aimed at bolstering Kenyan music, brings on board Sauti Sol's Bien". Citizen Digital (kwa Kiingereza). 2023-10-10. Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ Linda Wafula (2024-05-03). "Chiki Celebrates One Year of Managing Bien". KenyanVibe (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ "The Star". The Star (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ Nairobi Gossip Club. "Home". Nairobi Gossip Club (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2025-10-30.
- ↑ https://www.kbc.co.ke/bien-wins-trace-award-in-zanzibar/