Bidco

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nembo ya BIDCO

BIDCO ni mojawapo ya makampuni kubwa zaidi ya kutengeneza mafuta ya kupikia na vyombo vya sabuni katika eneo la Afrika Mashariki na Kati. Kituo kikuu cha Kampuni hii kiko mjini Thika, Kenya.

Historia[hariri | hariri chanzo]

BIDCO, iliyoanzishwa miaka 35 iliyopita na Bhimji Depar Shah. Jina BIDCO ilitolewa kutoka kwa mianzo B.D. (Bhimji Depar) pamoja na Co (Company).

Mukhtasari wa Kikundi cha Bidco[hariri | hariri chanzo]

  • 1970 Kiwanda cha Bidco cha Nguo
  • 1985 Kiwanda cha kutengenezea Sabuni Nairobi
  • 1991 Kiwanda cha kusafishia mafuta Thika
  • 1997 Yaongeza uwezo wake kwa asilimia 500.
  • 1998 Yanunua Elianto - Kiwanda cha kusagia mbegu za mafuta
  • 1999 Uwezo wa Elianto waongezwa kwa asilimia 400
  • 2001 Kiwanda cha Bidco Tanzania cha Mafuta na Sabuni
  • 2002 Yanunua Vitengo vyote vya Unilever vya mafuta ya kupikia
  • 2003 Mradi wa kiwanda cha kusafishia mafuta jijini Dar-es-salaam
  • 2003 Bidco Uganda yafunguliwa
  • 2004 Uwezo wa Elianto waongezwa hadi 30,000 'metric tonnes' kila mwaka
  • 2005 Kiwanda cha kutengenezea mafuta ya kupikia cha Jinja chafunguliwa
  • 2005 Shamba la miti ya aina ya 'Oil Palm' lazinduliwa
  • 2005 Bidco Uganda yapata tuzo la 'Gold Award' la 'Top Investor'

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]