Barnabas Kinyor

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Barnabas Kinyor (amezaliwa 3 Agosti 1961 kule Nandi Hills) ni Mkenya wa mbio za Mita 400 kuruka vizuizi.

Wasifu wa Kazi[hariri | hariri chanzo]

Alimaliza wa 7 katika Michezo ya Commonwealth ya 1990, wa nane katika Mashindano ya Dunia ya Riadha ya 1993]] katika shindano la mita 400 kuruka vizuizi la wanaume na akashinda Nishani ya Shaba katika Michezo ya Jumuia ya Madola ya 1994. Pia alishiriki shindano hilo katika Michezo ya Olimpiki ya 1992 na ile ya 1996, na pia Mashindano ya Dunia ya Riadha ya 1995 lakini hakufika finali.

Muda wake bora zaidi[hariri | hariri chanzo]

Muda wake bora zaidi ni sekunde 48.90, aliouweka wakati wa mashindano ya kupokezana vijiti ya Olimpiki ya 1992[1].

Maisha a Kibinafsi[hariri | hariri chanzo]

Ana mtoto mmoja wa Kiume Job Kinyor aliyezaliwa 1990[2]). Mwana huyu ni mwanariadha chipukizi wa Masafa ya katikati[3]. Pamoja na bibiye Salina Kosgei ambaye pia ni mwanariadha, wana watoto wawili: Billy (aliyezaliwa 1996) na Ruth (aliyezaliwa mnamo 2001)[4].

Virejeleo[hariri | hariri chanzo]

  1. World men's all-time best 400m hurdles (last updated 2001)
  2. IAAF profile for Job Kinyor. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-08-12. Iliwekwa mnamo 2010-01-13.
  3. Njenga, Peter. "Kenyan Trials lead to squad of 23 selections for Bydgoszcz", IAAF.org, 18 Juni 2008. Retrieved on 2008-06-23. 
  4. World Majors Marathon profile for Salina Kosgei. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-05-06. Iliwekwa mnamo 2010-01-13.
Makala hii kuhusu Mwanariadha wa Kenya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Barnabas Kinyor kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.