Nenda kwa yaliyomo

Bapsi Sidhwa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Bapsi Sidhwa (11 Agosti 193825 Desemba 2024) alikuwa mwandishi wa riwaya kutoka Pakistan aliyeandika kwa lugha ya Kiingereza na baadaye kuishi nchini United States.

Anajulikana zaidi kwa ushirikiano wake na mkurugenzi wa filamu wa Indo-Canada Deepa Mehta. Riwaya yake Ice Candy Man (1991) ilitumika kama msingi wa filamu ya Earth (1998). Pia riwaya yake Water: A Novel (2006) ilihamasisha filamu ya Water (2005).

Mwaka 2022, maisha yake yalionyeshwa katika filamu ya hali halisi iitwayo Bapsi: Silences of My Life, iliyotolewa na The Citizens Archive of Pakistan kupitia YouTube, ikiwa sehemu ya mfululizo wa hadithi za kizazi cha kwanza kuhusu mgawanyo wa India.[1]

  1. Asif Farrukhi (14 Julai 2012). "Cover Story: Review of The Crow Eaters in Urdu (includes an interview with Bapsi Sidhwa)". Dawn (newspaper). Iliwekwa mnamo 3 Novemba 2021.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bapsi Sidhwa kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.