Bahati Bukuku
Bahati Bukuku[1] (alizaliwa katika Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya, Oktoba 1981) ni mwimbaji wa nyimbo za Kiinjili na mwigizaji kutoka Tanzania anayejulikana kwa nyimbo kama vile Dunia Haina Huruma, [2] Songa Mbele, [3] Maamuzi Yako, Abneri, Wewe ni Mungu, Umewazidi Wote[4] na nyingine nyingi. Pia ameigiza katika baadhi ya sinema za Kikristo za Bongo na mwimbaji Jennifer Mgendi kama vile "Teke la Mama" na "Nipo Studio.[5]
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Bahati Bukuku alilelewa katika Mkoa wa Mbeya. [6] Alisoma katika shule ya msingi Muungano na shule ya Sekondari ya Meta.
Baada ya kumaliza sekondari, Bahati alihamia Dar es Salaam kwa ajili ya kurudia mtihani wake wa sekondari. Wakati huo ndipo alianza kuimba na hatimaye kurekodi albamu yake ya kwanza, Yashinde Mapito, ambayo ilimfanya ajulikane kote nchini.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Bahati Bukuku Biography, Career, Family, and Net worth ⚜ Latest music news online". mdundo.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-08-15.
- ↑ millardayo.com https://millardayo.com/taarifa-kuhusu-ajali-aliyoipata-bahati-bukuku/. Iliwekwa mnamo 2025-08-15.
{{cite web}}: Missing or empty|title=(help) - ↑ Wasafi Media (2022-05-29), BAHATI BUKUKU ARUDI UPYA KUPITIA WASAFI SUNDAY WORSHIP, iliwekwa mnamo 2025-08-15
- ↑ Bahati Bukuku (2016-11-07), Umewazidi Wote | Bahati Bukuku | Official Video, iliwekwa mnamo 2025-08-15
- ↑ "Jeniffer Mgendi: Kutoka uimbaji hadi uigizaji". Mwananchi (kwa Kiingereza). 2021-03-18. Iliwekwa mnamo 2025-08-15.
- ↑ "- YouTube". www.youtube.com. Iliwekwa mnamo 2025-08-15.