Nenda kwa yaliyomo

Baali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake ya mwaka 1500 KK hivi.

Baali (maana yake mmiliki au Bwana katika lugha za Kisemiti za Kaskazini zilizotumika huko Mashariki ya Kati ya kale) ni jina lililokuja kutumika kwa ajili ya miungu, hasa kwa mungu wa dhoruba na wa uzazi, Hadad.

Biblia ya Kiebrania inalitumia mara 90 kuhusiana na miungu mbalimbali ya makabila jirani na Waisraeli waliosadiki Mungu mmoja tu na kuona hiyo mingine kuwa miungu bandia tu. Biblia inaeleza ibada za makuhani wa Baali [1], na hasa shindano lililoitishwa na nabii Eliya juu ya mlima Karmeli ili kuwaonyesha Waisraeli yupi ni Mungu wa kweli kati ya YHWH na Baali dhidi ya juhudi za malkia Jezebeli za kueneza kati yao dini ya taifa lake (Tiro) [2].

Matumizi hayo yaliingia katika Ukristo[3] na Uislamu[4], pengine kwa umbo la dharau Beelzebub, kuhusu pepo.

  1. 2Fal 10:22; 23:5
  2. 1Fal 18
  3. Math. 12:24, 27; Mk. 3:22; Lk. 11:15, 18f.), kama jina lingine la shetani: Math. 12:26; Mk. 3:23, 26; Lk. 11:18
  4. Quran Sura 37, 123-132

Marejeo mengine

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.