Ayisat Yusuf
Mandhari
Ayisat Yusuf-Aromire (alizaliwa 6 Machi 1985) ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa wanawake kutoka nchini Nigeria, ambaye sasa anaishi Ufini.
Yusuf alicheza kwenye klabu kadhaa nchini Nigeria na Ufini, na alikuwa sehemu ya kikosi cha Nigeria kilichoshiriki katika Mshindano wa Mabingwa wa Afrika wa Wanawake 2004, Kombe la Dunia la Wanawake 2007, na Michezo ya Olimpiki ya 2008.
Baada ya kustaafu kutoka soka la ushindani, aliishi Finland na kuanza kufanya kazi kama kocha wa soka na pia mchambuzi wa kijamii akisaidia wanawake na wasichana wakimbizi kupitia michezo.
Yusuf anaishi Kannelmäki, Helsinki, na ameolewa na mwanamume mmoja wa Nigeria. Watoto wao wote walizaliwa Ufini.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Instructors - Fit4Life". www.fit4life.fi. Iliwekwa mnamo 2025-07-20.
| Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ayisat Yusuf kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |