Ayaan Hirsi Ali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ayaan Hirsi Ali (2016)

Ayaan Hirsi Ali (kwa Kisomali: Ayaan Xirsi Cali: Ayān Ḥirsī 'Alī; alizaliwa: Ayaan Hirsi Magan, huko Somalia, 13 Novemba 1969)[1] ni mwanaharakati wa haki za wanawake, mwandishi, msomi na mwanasiasa wa zamani raia wa Uholanzi na Marekani.[2][3]

Alipata usikivu wa kimataifa kwa kuwa mkosoaji wa Uislamu na mtetezi wa haki za wanawake wa Kiislamu, akipinga kwa nguvu ndoa za kulazimishwa, mauaji ya heshima, ndoa za utotoni na ukeketaji wa wanawake.[4][5]Alianzisha shirika la kulinda haki za wanawake liitwalo AHA Foundation. Ayaan Hirsi Ali hufanya kazi kwa ajili ya Hoover Institution na American Enterprise Institute.[6][7]

Mnamo mwaka 2003, Hirsi Ali alichaguliwa kuwa mwanachama wa baraza la wawakilishi la Uholanzi.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ayaan Hirsi Ali kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.