Avito wa Vienne

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake huko Drome.

Avito wa Vienne (kwa Kilatini: Alcimus Ecdicius Avitus; Vienne, Ufaransa, 450 hivi – 5 Februari 523) alikuwa mshairi halafu askofu mkuu wa mji huo kuanzia mwaka 494.

Ni maarufu kwa imani na juhudi zake ambazo aliweza kumaliza Uario kati ya Waburgundi na kuwavuta katika Kanisa Katoliki, pamoja na kukinga Galia nzima dhidi ya uzushi huo.

Baba yake alikuwa seneta, halafu askofu wa Vienne. Vilevile mdogo wake Apolinari alipata kuwa askofu wa Valence.

Tangu zamani anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Februari[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

Barua[hariri | hariri chanzo]

  • Avitus of Vienne, Selected Letters and Prose. Tr. by Danuta Shanzer and Ian Wood. Liverpool: Liverpool University Press, 2002, 464 pp. (Translated Texts for Historians).

Mashairi[hariri | hariri chanzo]

  • Avitus, The Fall of Man: De spiritalis historiae gestis libri I-III, Edited from Laon, Bibliothèque Municipale, Ms. 273. Edited by Daniel J. Nodes. Toronto: Pontifical Institute of Medieval Studies, 1985, 72 pp. (Toronto Medieval Latin Texts, 16).
  • Avit de Vienne, Histoire spirituelle, Tome II: (Chants IV-V). Edited by Nicole Hecquet-Noti. Paris: Les Editions du Cerf, 2005, Pp. 254. (Sources Chretiennes, 492).
  • M. Hoffman. 2005. Alcimus Ecdicius Avitus. De spiritalis historiae gestis Buch 3 (Munich: K.G. Saur).
  • George W. Shea (trans.), The Poems of Alcimus Ecdicius Avitus (Tempe, Ariz.: Medieval & Renaissance Texts & Studies, 1997).
  • Avitus, De mundi initi, ed. by Abraham Schippers (Kampen: Kok, 1945).

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.