Apiani wa Kaisarea

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Mt. Apiani.

Apiani wa Kaisarea (Lycia, leo nchini Uturuki, 287 hivi - Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 305 hivi) alikuwa kijana msomi ambaye aliongokea Ukristo.

Kwa sababu ya imani yake, alijaribu kuzuia ibada ya Kipagani, ambayo Wakristo walilazimishwa kuishiriki katika dhuluma ya kaisari Masimino Daia: alimkaribia kishujaa gavana Urbano na kumshika mkono. Hapo akachomwa moto miguu na kutoswa na askari baharini [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadimishwa tarehe 2 Aprili[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.