Antasari Azhar
Antasari Azhar (18 Machi 1953 – 8 Novemba 2025) alikuwa mwenyekiti wa zamani wa Tume ya Kupambana na Ufisadi ya Indonesia. Alifukuzwa kazi mnamo 11 Oktoba 2009 baada ya kuhukumiwa kwa mauaji. Mwanzoni mwa 2017, alipata msamaha wa Rais Joko Widodo akaachiwa huru.[1][2][3][4]
Elimu
[hariri | hariri chanzo]Antasari alizaliwa Pangkal Pinang, kisiwa cha Bangka, akakulia kisiwa cha Belitung. Baada ya kumaliza shule ya msingi mwaka 1965, aliendelea na shule ya sekondari mjini Jakarta, na kuhitimu mwaka 1971. Baadaye alisoma Chuo Kikuu cha Sriwijaya, akichagua masomo ya usimamizi wa serikali na kumaliza mwaka 1981. Wakati akiwa chuoni, Antasari alikuwa Mwenyekiti wa Seneti na Kiongozi wa Jumuiya ya Wanafunzi. Alishiriki katika maandamano mwaka 1978. Baadaye, akiwa wakili wa serikali, alichukua kozi kadhaa ikiwa ni pamoja na Sheria ya Biashara katika Chuo Kikuu cha New South Wales huko Sydney, na Uchunguzi wa Sheria ya Mazingira katika Mamlaka ya Ulinzi wa Mazingira huko Melbourne.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Jokowi Grants Antasari Azhar Clemency". Jakarta Globe. 26 Januari 2017.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "view the location of this item Indonesian prosecutor convicted for murder". Radio Netherlands Worldwide. 11 Februari 2010.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Profil Antasari Azhar - VIVA". www.viva.co.id (kwa Kiindonesia). 2016-11-07. Iliwekwa mnamo 2024-06-06.
- ↑ "d the High State Prosecutor's Office". Jakarta Globe. 20 Desemba 2009.
{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Antasari Azhar kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |