Anna Lührmann

Anna Lührmann (alizaliwa mnamo tarehe 14 Juni 1983) alikuwa mwanasayansi wa siasa kutoka Ujerumani na mwanasiasa wa Muungano 90/Wa-Kijani ambaye alihudumu kama mbunge wa Bundestag kufuatia Uchaguzi wa shirikisho la Ujerumani wa mwaka 2021.[1]
Mbali na kazi yake ya ubunge, alikuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Mambo ya Nje ya Shirikisho ndani ya Baraza la Mawaziri la Scholz kuanzia tarehe 8 Desemba 2021.[2][3]
Lührmann alikuwa mbunge mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kuchaguliwa katika Bundestag mwaka 2002, na pia alikuwa mbunge mwenye umri mdogo zaidi duniani wakati huo. Kama msomi, aliwahi kuwa naibu mkurugenzi wa Taasisi ya V-Dem na profesa msaidizi katika Chuo Kikuu cha Gothenburg.
Alirejea kwenye siasa mwaka 2021, na aliwakilisha jimbo la Rheingau-Taunus-Limburg katika Bundestag.
Mzaliwa wa Lich, jimbo la Hesse, wakati huo sehemu ya Ujerumani Magharibi, Lührmann alijiunga na Chama cha Kijani akiwa na umri wa miaka 13, baada ya kushiriki katika harakati za Grün-Alternative Jugendbündnis, tawi la vijana wa chama hicho.
Kazi ya kitaaluma
[hariri | hariri chanzo]Mnamo Oktoba 2023, Lührmann alishiriki katika mkutano wa kwanza wa pamoja wa Baraza la Mawaziri kati ya serikali za Ujerumani na Ufaransa uliofanyika Hamburg, chini ya uenyekiti wa Chansela Olaf Scholz na Rais Emmanuel Macron.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Jan Dams (14 June 2007), Forschungsministerin bleibt auf 246 Millionen Euro sitzen Berliner Morgenpost.
- ↑ Ulrike Winkelmann (30 May 2008), [Jung-Abgeordnete Lührmann hört auf: "Die Gefahr, Apparatschik zu werden"] Die Tageszeitung.
- ↑ Mathias Hamann (25 September 2009), Abgang von Anna Lührmann, MdB: "Manchmal hat sie genervt" Der Spiegel.
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Anna Lührmann kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |