Angel Wainaina
Angela "Angel" Wainaina (1983 – 28 Januari 2009) alikuwa mwigizaji, mtangazaji wa redio na msanii wa muziki wa kufokafoka(rap) kutoka Kenya.
| Angela Wainaina | |
|---|---|
| Amezaliwa | 1983 Nairobi, Kenya |
| Amekufa | 28.01.2009 Nairobi, Kenya |
| Kazi yake | Muigizaji |
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Wainaina alizaliwa mwaka 1983 huko Kawangware, maeneo duni ya makazi jijini Nairobi, Kenya. Aliungana na kikundi cha maigizo katika shule ya sekondari ya Kambui. Alikuwa mshindi wa pili katika shindano la Miss Kenya mwaka 2005. Pia alikuwa mshairi na msanii wa kufokafoka(rap) wa chini. Aliigiza kama Sajenti Maria katika kipindi maarufu cha televisheni Cobra Squad.[1]
Tarehe 15 Januari 2007, alianza kufanya kazi katika Ghetto Radio, akiwa mtangazaji wa kwanza mwanamke nchini Kenya. Kipindi chake “Chanuka Dada” kilikuwa maarufu sana, na alijulikana kwa uanaharakati wake wa kijamii uliokuwa na nguvu. Alitunukiwa tuzo ya vyombo vya habari ya Young Women African Summit.
Kifo
[hariri | hariri chanzo]Wainaina alifariki dunia tarehe 28 Januari 2009 kwa moto wa duka kubwa la Nakumatt. Mazishi yake yalifanyika katika Kanisa Kuu la Holy Family jijini Nairobi.[2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Angel Wainaina kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |