Andreas Brehme
Andreas “Andi” Brehme 9 Novemba 1960 – 20 Februari 2024) alikuwa mchezaji wa mpira wa miguu wa kulipwa na kocha kutoka Ujerumani. Katika kiwango cha kimataifa, anajulikana zaidi kwa kufunga bao la ushindi kwa Ujerumani katika fainali ya Kombe la Dunia la FIFA 1990 dhidi ya Argentina kupitia mkwaju wa penalti dakika ya 85. Katika ngazi ya klabu, Brehme alichezea timu kadhaa nchini Ujerumani na pia alipata vipindi vya kucheza nchini Italia na Hispania.
Akiwa beki wa pembeni mwenye uwezo wa kushambulia na jicho la kufunga mabao, Brehme aliweza kucheza sehemu yoyote ya pembeni mwa uwanja, upande wa kushoto au kulia. Alijulikana kwa uwezo wake wa kupiga krosi, kutumia miguu yote miwili kwa ustadi, na umakini wake katika mipira ya adhabu ndogo (free-kicks) na penalti, akiwa na shuti lenye nguvu.[1]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ LUIGI PASTORE (7 Oktoba 2001). "L' orgoglio di Ferri 'È un' Inter solida'". La Repubblica (kwa Kiitaliano). Iliwekwa mnamo 5 Novemba 2017.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
| Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Andreas Brehme kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |