Andrea Corsini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Andrea Corsini akisali - Guido Reni (1630-1635).

Andrea Corsini, O.Carm. (30 Novemba 13026 Januari 1373/1374) alikuwa Mkarmeli wa Italia aliyehudumia kama askofu wa Fiesole tangu mwaka 1349 hadi kifo chake.

Akiwa kijana aliishi vibaya hadi karipio la mama yake lilipomfanya aamue kuingia utawani aliposhika maisha magumu na kutafakari sana Biblia.

Baada ya kushika nafasi mbalimbali shirikani, akirekebisha konventi zilizoharibiwa na tauni, alikubali kwa shida uaskofu akaongoza kwa busara jimbo lake akiongeza juhudi zake za kiroho na matendo ya huruma kwa maskini na kupatanisha maadui.

Tangu kale aliheshimiwa na waumini na hatimaye Papa Eugenio IV alimtangaza mwenye heri tarehe 21 Aprili 1440 na Papa Urban VIII alimtangaza mtakatifu tarehe 22 Aprili 1629.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Attwater, Donald and Catherine Rachel John. The Penguin Dictionary of Saints. 3rd edition. New York: Penguin Books, 1993. ISBN|0-14-051312-4.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.