Amna Elhassan
| Amna Elhassan | |
|---|---|
| Amezaliwa | 1988 |
| Elimu | Chuo Kikuu cha Khartoum; Chuo Kikuu cha Sapienza, Roma, Italia |
| Kazi yake | Mchoraji |
| Tovuti | |
| https://www.amnaelhassan.com/ | |
Amna Elhassan (alizaliwa mwaka 1988 huko Khartoum, Sudan) ni msanii wa sanaa ya kuona kutoka Sudan na mbunifu wa majengo aliyesomea taaluma hiyo, ambaye anaishi na kufanya kazi mjini Khartoum. Kazi zake za kisanaa mara nyingi hujikita katika mtazamo na nafasi ya wanawake wa Kisudan katika maisha ya umma na ya binafsi, na huwasilishwa kupitia vyombo mbalimbali vya sanaa, ikiwemo uchapaji wa michoro na uchoraji wa picha
Maisha na uzoefu wa kazi
[hariri | hariri chanzo]Mnamo mwaka 2010, Elhassan alipata shahada ya kwanza ya usanifu majengo kutoka Chuo Kikuu cha Khartoum. Baadaye, mwaka 2013, alipata shahada ya uzamili ya usanifu wa majengo katika Chuo Kikuu cha Sapienza huko Roma, Italia. Baada ya kurejea Sudan, alijikita katika sanaa za uchoraji na sanaa za faini, akifanya kazi pamoja na mlezi wake, msanii wa Kisudan Hatim Koko, katika Kituo cha Mafunzo ya Sanaa cha Khartoum. Maonyesho yake ya kwanza ya sanaa yalifanyika mjini Khartoum katika Kituo cha Sanaa cha Rashid Diab na Makumbusho ya Taifa ya Sudan.
Miongoni mwa maonyesho mengine, tangu mwaka 2016 na kuendelea. Zaidi ya hayo, ameonyesha kazi zake katika maonyesho kadhaa ya kimataifa, na mnamo Julai 2022 alialikwa kama mhadhiri mgeni katika Chuo cha Sanaa za Faini cha Hamburg, Ujerumani, akifundisha darasa lililopewa kichwa cha “Sanaa Wakati wa Mgogoro”[1].Kazi zake pia ziliwasilishwa katika kitabu cha sanaa cha 2019 kilichoitwa Sudan Retold, kama sehemu ya kundi la wasanii vijana wanaoeleza matoleo yao ya kisanaa ya historia, hali ya sasa, na mustakabali wa Sudan.[2]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]
| Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Amna Elhassan kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |